Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mradi wa maji Sumve, Malya na Malampaka baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwanza kabisa ninamshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Naomba uniruhusu nimshukuru Mheshimiwa Rais wangu ametupatia fedha shilingi bilioni 440 kwa ajili ya mradi wa Ziwa Victoria kuleta Simiyu na Wilaya zake Busega, Bariadi, Itilima, Maswa na Meatu, mkataba tumesaini juzi tarehe 27 mwezi wa Tano. Ahsante sana Mama yangu.

Mheshimiwa Spika, swali dogo, kwa kuwa Mkoa wa Simiyu ni Mkoa wa wafugaji; je, napenda kujua mradi huu utahudumia na upande wa mifugo pia? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, namshukuru kwa kutambua jitihada za Mheshimiwa Rais na tutaendelea kuunga jitihada zake kwa kuhakikisha tunasimamia vema fedha zote ambazo anazielekeza kwenye miradi hii mikubwa. Kuhusiana na mifugo wakati Mheshimiwa Waziri akisaini mradi huu mkubwa alioshukuru Mheshimiwa Mbunge Esther, tayari tumetenga malambo sita kwa ajili ya mifugo, hivyo mifugo pia itanufaika. (Makofi)

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mradi wa maji Sumve, Malya na Malampaka baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba mradi wa kutoa maji kutoka Mto Mafumbo kwenda kwenye Mji wa Mlowo na Vwawa unatekelezwa kwa haraka, ili kuondoa adha ya wakazi wa Mlowo na Vwawa wanaokabiliwa na tatizo kubwa la uhaba wa maji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole, Mbunge wa Mbozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mto Mafumbo ni moja ya chanzo kilichogunduliwa na Ofisi yetu ya Bonde la Ziwa Tanganyika na tayari Ofisi ya Vwawa - Mlowo wanashughulika na chanzo hiki kuhakikisha kiweze kutumika. Wameshaandika proposal imekuja Wizarani, ninaahidi tutafanyia kazi kwa sababu ya umuhimu wake. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mradi wa maji Sumve, Malya na Malampaka baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Natambua zaidi ya bilioni 10 zimetumika katika mradi wa maji Bunda kutoka Nyabeu kuleta Mjini. Bado kuna tatizo la usambazaji katika Kata zote 14, tunahitaji shilingi bilioni saba ili kata zote 14 zipate huduma ya maji safi na salama.

Ni lini sasa Serikali mtakamilisha usambazaji? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maeneo haya aliyoyataja Kata Saba tayari kama Wizara tunayafanyia kazi na usanifu unaendelea, tutahakikisha usambazaji hautachukua muda utakamilika ndani ya wakati. (Makofi)