Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Water and Irrigation Wizara ya Maji 489 2023-05-31

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:-

Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mradi wa maji Sumve, Malya na Malampaka baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa miradi ya maji Sumve, Malya na Malampaka kupitia chanzo cha maji cha Ziwa Victoria. Mji wa Sumve utapata maji kupitia mradi wa maji Ukirugulu – Usagala – Kolomije hadi Sumve. Mkandarasi yupo eneo la mradi anaendelea na kazi. Aidha, Miji ya Malya na Malampaka itapata maji kupitia mradi wa maji wa Hungumalwa na Mkandarasi ameajiriwa mwezi Mei, 2023.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo, na Serikali itaendelea kutenga fedha kila mwaka hadi kukamilika kwa miradi hiyo.