Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, lini Serikali itatenga maeneo ya malisho ya mifugo katika Pori la Usumbwa Forest Reserve?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante, wananchi wa Ushetu wanaheshimu sana mipaka ya Serikali kwenye mapori yetu na ni walinzi wazuri sana, lakini idadi ya ng’ombe wa wananchi wa Ushetu inazidi kuongezeka. Mpaka sasa Wananchi wa Ushetu wana ng’ombe 176,000 na wanapakana na mapori haya hawana kabisa eneo la kuchungia.

Je, Serikali itamaliza lini hii tathmini ili wananchi hawa waweze kupata sehemu ya kulishia mifugo yao, badala ya kuendelea kugombana na watu wa maliasili?

Swali langu la pili, Halmashauri ya Ushetu ina mapori matatu. Inayo pori la Usumbwa Forest Reserve, Ubagwe Forest Reserve pamoja na Mpunze Saba Sabini, lakini Ubagwe Forest Reserve imekuwa na mgogoro mkubwa sana na Halmashauri ya Kaliua ambao umechukua sura mpya. Hata juzi wananchi wangu wamekamatwa wakawekwa ndani bila sababu za msingi, mbaya zaidi juzi kumekuwa na mgogoro kati ya maliasili wa TFS na Askari wa Maliasili wa Ushetu, Mheshimiwa Naibu Waziri huo mgogoro anaujua nilimtaarifu.

Nini kauli ya Serikali na Mheshimiwa Waziri ni lini tutaenda kutatua mgogoro huu kwa wananchi wangu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Katika eneo hili la kulishia mifugo, ninaendelea tu kumshauri Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Ushetu kwamba, kwa kuwa Wizara ya Maliasili imepewa dhamana ya kuyalinda na kuyasimamia maeneo haya, inapofika suala la mahitaji ya maeneo ya mifugo basi waendelee kuwasiliana na Wizara husika ili tukae Pamoja, tuone namna iliyo bora ya kutenga maeneo haya, tumepewa kazi ya kuyasimamia tu na kuyatunza maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, suala lingine hili la kuhusu mipaka na migogoro kati ya TFS na Pori la Usumbwa Forest Reserve tunaendelea kuangalia namna ya kuainisha mipaka na kwa kuwa sote ni Serikali moja kwa maana ya Halmashauri na TFS, hakuna haja ya kugombania mipaka isipokuwa ni masuala ya kiutawala tu kwamba hawa ni TFS na hawa ni Halmashauri ni kukaa pamoja tu ili sote tulinde haya mapori kwa pamoja.