Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 488 2023-05-31

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:-

Je, lini Serikali itatenga maeneo ya malisho ya mifugo katika Pori la Usumbwa Forest Reserve?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mahitaji ya Wananchi wa Ushetu na inaendelea kufanya tathmini ya eneo la Msitu wa Usumbwa Forest Reserve ili kujiridhisha kama unastahili kumegwa kwa ajili ya kutengwa eneo la kuchungia. Pindi tathmini itakapokamilika wananchi watajulishwa. Wakati Serikali inaendelea na tathmini hiyo wananchi wanashauriwa kuendelea kuheshimu maeneo hayo ili kuhifadhi msitu huo.