Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza:- Je, lini Serikali itaanzisha Benki ya Vijana Wajasiriamali?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa hii, naomba sasa niulize swali dogo la nyongeza.

Kwanza naipongeza Serikali kwa majibu mazuri, kwa kuwa katika mkutano wa vijana Mkoa wa Mwanza na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliahidi kwamba tutaanzisha Benki ya Vijana Wajasiriamali.

Je, ningependa kufahamu ni hatua zipi zimefikiwa katika mchakato wa uanzishwaji wa benki hiyo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, awali ya yote naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Lucy pamoja na Wabunge wengine wote kwa kufuata nyanyo za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutaka kujua au kuona hali ya vijana wetu kiuchumi inaimarika.

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sabu kwamba suala hili lipo katika hatua ya majadiliano katika kikao kazi cha Makatibu Wakuu, litakapokamilika tu hatua iliyopo sasa, basi tutajulishwa ili wananchi wote wajue na hatua nyingine ziweze kuendelea.