Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 487 2023-05-31

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanzisha Benki ya Vijana Wajasiriamali?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa uwezeshaji vijana kiuchumi, Serikali ipo katika hatua ya kuandaa mkakati wa upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali wadogo na wa kati, ambao utawezesha vijana kupata mitaji kupitia benki, taasisi za huduma ndogo za fedha, masoko ya mitaji, mifuko na programu za Serikali za uwezeshaji wananchi kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, katika hatua ya utekelezaji wa mkakati huu, Serikali inatarajia kuanzisha taasisi mahsusi ya fedha itakayosimamia upatikanaji na utoaji wa mikopo kwa makundi maalum wakiwemo vijana, wanawake, watu wenye ulemavu na wafanyabiashara wadogo wadogo wakiwemo wamachinga. Ahsante.