Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:- Je, lini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Serya utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, ninakushuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu yenye kuridhisha ya Serikali nataka kujua sasa, Je, hizo shilingi milioni 300 ambazo zilitengwa kwa kufanya kazi zilizotajwa na Mheshimiwa Waziri hapo, zilitolewa na zikafanya kazi iliyokusudiwa ama walifanya tafiti tu za awali?

Swali la pili, kwa kuwa Serikali ina makusudio ya kufanya kuanza ujenzi mwaka ujao wa fedha, kwa kazi ya kuhuisha sasa hii skimu na hizi ripoti na tafiti, Wizara safari hii imetenga kiasi gani kwa ajili ya kazi hii? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu matumizi ya fedha shilingi milioni 300 kama zilitoka au la. Madhumuni makubwa ya fedha hizi zilikuwa ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ndiyo maana katika majibu yangu ya msingi nimesema katika kupata tathmini halisi, tumetenga fedha tena mwaka huu kuhakikisha ya kwamba tunalipitia eneo lote ili kupata taarifa sahihi na kuanza ujenzi wake kwa sababu tumepata changamoto miradi mingi ilipata changamoto kubwa, kwa sababu usanifu wa kina haukufanyika na imekuwa siyo ya kudumu muda mrefu na hivyo kuleta athari kubwa kwa sababu mara kwa mara imekuwa ikibomoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tunakwenda kurudia kufanya kazi hii kubwa katika umakini mkubwa zaidi na ku-involve wataalam wengi zaidi ili tupate kitu ambacho kitaleta tija kwa wananchi wa Kondoa Mjini.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kuhusu fedha kama zimetengwa. Kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ya kwamba tunajiandaa kufanya zoezi hili katika mwaka wa fedha 2023/2024 ili ujenzi uanze katika mwaka wa fedha unaokuja 2024/2025. Kwa hiyo, nimtoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaangalia namna ya kuweza kulifanikisha kwa uharaka kwa sababu tunajua wananchi wa Serya na eneo la Mongoroma ni wakulima wazuri hatutaki kuwachelewesha, tutafanya kwa uharaka ili wafanye kilimo cha umwagiliaji katika eneo lao. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:- Je, lini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Serya utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Umwagiliaji Muhuruzi - Nyakahura Wilaya ya Biharamulo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwenye kitabu chetu cha bajeti, kiambatisho Namba 11 Ukurasa wa 206 tumeitaja Skimu ya Muhuruzi katika Wilaya ya Biharamulo kama sehemu ambazo zitajengwa katika mwaka huu wa fedha unaoanza Julai. Kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kazi inafanyika katika mwaka wa fedha ujao.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:- Je, lini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Serya utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika Halmashauri ya Kasulu Vijijini ipo miradi ya umwagiliaji katika Kata ya Titye na Rungwe Mpya. Miradi hiyo haijakamilika kutokana na ukosefu wa fedha.

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kukamilisha miradi hiyo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kazi ya kwanza ambayo tuliifanya kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ni kuhakikisha tumepitia miradi yote ambayo haijakamilika na ili tujue changamoto ambazo zimefanya imekwama na tuweze kuikwamua. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba katika orodha ya miradi hiyo, miradi anayoitaja pia imo. Tutaikwamua ili wananchi wafanye kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)