Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 486 2023-05-31

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji katika Kata ya Serya utaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kata ya Serya iliyopo katika Tarafa ya Kondoa Mjini ipo takriban kilometa 20 kutoka Kondoa Mjini. Mwaka 2007, Vijiji vya Mongoroma na Serya vilitenga eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji lenye ukubwa wa hekta 3000. Pia Kijiji cha Mongoroma kilitenga eneo la ujenzi wa bwawa ambalo linapakana na eneo la pori la hifadhi ambalo lilikuwa tayari na aina mbalimbali za wanyama. Skimu inatarajiwa kutumia maji ya mvua pamoja na kuchepusha maji ya Mto Bubu na kuyahifadhi kupitia ujenzi wa Bwawa la Mongoroma. Eneo hili linastawisha mazao mbalimbali yakiwemo mahindi, mtama, mbaazi na mbogamboga zinazolimwa kwa kiwango kidogo pembezoni mwa Mto Bubu kwa njia ya Umwagiliaji wa kutumia pampu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2010/2011, Serikali kupita Mfuko wa Kuendeleza Kilimo cha Umwagiliaji ngazi ya Wilaya chini ya ASDP 1 ilitenga fedha kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina wa bwawa na skimu, pamoja na maandalizi ya awali ya jamii husika katika kushiriki katika ujenzi wa Skimu na Bwawa la Mangoroma/Serya.

Mheshimiwa Spika, aidha, kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, ongezeko la watu na makazi kufuatia kasi ya kukua kwa Mji wa Kondoa eneo la bwawa kupakana na hifadhi Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, kwa kushirikiana na Halmashauri ina mpango wa kuhuisha tafiti za awali zilizofanyika mwaka 2010/2011 pamoja na kufanya utafiti mpya wa athari za mazingira na jamii, matokeo ya uhuishaji wa tafiti hizo, yataiwezesha Serikali katika mwaka wa fedha 2024/2025 kutega fedha za ujenzi wa Bwawa na Skimu ya Mongoroma/Serya.