Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza tija katika uzalishaji wa zao la Pareto Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri yenye kutia matumaini, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Serikali imekiri kwamba upatikanaji wa pembejeo ndiyo shida mojawapo inayofanya zao hili lisilete tija iliyokusudiwa. Je, Serikali haioni pamoja na kwamba mwakani itatusambazia hizo mbegu bure, je na pembejeo zingine kama mbolea tutazipata?

Swali la pili, kwa kuwa tunayo Bodi ya Pareto, je, Serikali haioni umuhimu wa kuiwezesha hiyo Bodi ya Pareto kwa kuwaongeza bajeti na kuwaongezea watumishi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema pamoja na usambazaji wa miche bora ambayo itasaidia katika kuongeza tija pia wakulima wa pareto wanaingia katika mpango wa mbolea ya ruzuku. Kwa hiyo ni wanufaikaji na watanufaika pia kupitia mbolea hii.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kuhusu bajeti kwenye Bodi ya Pareto tunaendelea kulifanyia kazi suala hili, tumeendelea kuijengea Bodi uwezo tofauti na miaka miwili iliyopita, lengo letu ni kulikuza zao la pareto ambalo limekuwa na manufaa makubwa. Kwa hiyo, Bodi tutawajengea uwezo kuhakikisha kwamba bajeti yao inaongezeka pia. (Makofi)