Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 485 2023-05-31

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza tija katika uzalishaji wa zao la Pareto Wilayani Kilolo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Justin Lazaro Nyamoga, Mbuge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tija ya sasa ni kati ya kilo 280 hadi 300 ya pareto kavu kwa ekari. Hata hivyo, tija inayoweza kufikiwa na wakulima wengi ni kati ya kilo 400 hadi 500 kwa ekari moja. Pamoja na mambo mengine tija ndogo inasababishwa na wakulima wengi kwa muda mrefu kuendelea kutumia mbegu ambazo zina tija ndogo na wakulima walio wengi kutopendelea kutumia mbolea katika uzalishaji wa zao la pareto.

Mheshimiwa Spika, aidha, kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo katika mwaka wa fedha 2022/2023 ilitenga fedha kiasi cha shilingi milioni 200 ambazo zilipelekwa TARI kwa ajili ya kuzalisha mbegu bora na zenye tija. Upatikanaji na usambazaji wa mbegu bora hizo unatarajiwa kuanza msimu 2023/2024. Mbegu hizo ambazo zitakuwa na tija kuanzia kilo 400 na zaidi kwa ekari zitasambazwa kwa wakulima wote wa pareto nchini ikiwa ni pamoja Wilaya ya Kilolo. Usambazaji huo utaenda sambamba na utoaji elimu ya mbinu bora za kilimo cha pareto kwa wakulima ikiwa ni pamoja na kuendesha tafiti za matumizi ya mbolea kwa zao la pareto. Utoaji wa elimu utafanywa kwa ushirikiano kati ya Serikali na Sekta Binafsi hususan Wanunuzi na Wasindikaji wa zao katika Wilaya ya Kilolo.