Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Nyagokolwa, Mbogo na Mhuze Wilayani Itilima?

Supplementary Question 1

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na jinsi walivyojibu katika swali la msingi. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika Daraja la Mto Garamoha ni daraja linalounganisha Kata tatu, Kata ya Mwaswale, Nkuyu na Ndolelezi na daraja lile hupelekea kipindi cha mvua wananchi kushindwa kupita katika eneo hilo kwenda kupata huduma katika Kata ya Sagata. Sasa kwa kuwa fedha ni kiasi kidogo cha bajeti ya TARURA kwa nini Serikali isiweke kwenye fedha za maendeleo ili kusudi wananchi waweze kujengewa daraja hilo?

Swali la pili, kwa kuwa katika Kata ya Mwaswale kuna barabara ambayo TARURA wamejenga kutoka Makutano hadi Mwakubija lakini bado kilomita 51 za kutoka Mwakubija kwenda Sopalodge. Serikali sasa haioni umuhimu wa kufungua barabara ya kutoka Mwakubija kwenda Sopalodge kwa ajili ya kwenda kufanya shughuli za kiutalii katika Wilaya hii ya Itilima? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Silanga swali lake la kwanza kuhusu fedha iliyotengwa kwa ajili ya daraja hili la Mto Garamoha, tutaangalia katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 tuone fedha hii iliyotengwa kwa ajili ya ujenzi wa daraja hii inakwenda mara moja ili kuweza kujenga daraja hili kuweza kutoa huduma kwa wananchi wa maeneo aliyoyataja Mheshimiwa Silanga.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la kujenga barabara hii ya kilometa 51 kutoka Maswale kuelekea Sopalodge. Barabara hii tayari ujenzi wake ulikuwa umeshaanza hapo awali na kwa sasa hii barabara inapita katika Pori Tengefu la Maswa katika maeneo ya Nyasosi kuelea Sopalodge ambapo barabara kufika Nyasosi pale wameishia pale na bado hizo kilometa 51. Kwa sababu barabara hii ni muhimu sana ambayo inafupisha wananchi wa maeneo haya badala ya kuzunguka kilometa 250 wanakuwa wanaenda chini ya kilometa 100 kufika katika maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, tutaendelea kuipa kipaumbele kadri ya upatikanaji wa fedha ili tuweze kujenga barabara kuanzia Gwalali kuelekea Makutano hadi kufika Mwakibija na kuelekea kule Sopalodge.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Nyagokolwa, Mbogo na Mhuze Wilayani Itilima?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga madaraja ya kuunganisha Jimbo la Mbagala na Jimbo la Mkuranga?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kujenga madaraja ya kuunganisha Wilaya hizi mbili au Mikoa hii miwili, Mkoa wa Pwani na Mkoa wa Dar es Salaam. Kwa sasa, tumeweka daraja la Mto Kitonga kuhakikisha katika mradi wa DMDP II ambapo fedha hizi zitakapopatikana kuanzia mwaka wa fedha huu Novemba, 2023 tutaanza utekelezaji wa kujenga daraja hili. Barabara hii ni ya muhimu sana kwa sababu kuna huduma nyingi za mchanga unaotoka katika Wilaya ya Mkuranga kuelekea Mkoa wa Dar es Salaam inapita katika barabara hii.

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Nyagokolwa, Mbogo na Mhuze Wilayani Itilima?

Supplementary Question 3

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa, wananchi wa Kata ya Mwamanga Kijiji cha Mwamanga, Inolelo na Kisasa B, wanapata shida sana wakati wa mvua kwenda kwenye huduma hasa wanafunzi wa sekondari. Je, Serikali ina mpango gani wa kutupa fedha kwa ajili ya kujenga barabara na daraja hili kuunganisha hasa bottleneck ili wananchi wapate huduma hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nitakaa na Mheshimiwa Kiswaga tuone katika bajeti ya 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi huu wa daraja katika Kata ya Mwamanga kule Wilayani Magu na kama haijatengewa fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024 basi tutaangalia kutenga fedha kwenye mwaka wa fedha 2024/2025.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Nyagokolwa, Mbogo na Mhuze Wilayani Itilima?

Supplementary Question 4

MHE. CHATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Je, ni lini Serikali kupitia TARURA itajenga Daraja la Mto Juwe kuunganisha Kijiji cha Eyasi, Mdito, Oldonyosambu na Jema Wilayani Ngarongoro Mkoa wa Arusha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeanza usanifu wa Daraja la Mto Juhe katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kupitia Wakala wa Barabara Vijijini (TARURA) na ilikuwa imetengwa shilingi milioni 200 kama na nane hivi, kwa ajili ya usanifu na ujenzi wa madaraja na makaravati katika barabara hii ambayo inapita katika eneo hili la Mto Juhe.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Nyagokolwa, Mbogo na Mhuze Wilayani Itilima?

Supplementary Question 5

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja la Mto Nyahende kule Nyansulula?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la Mheshimiwa Amsabi Mrimi la Mto Nyahende kule Wilayani Serengeti tutaangalia katika mwaka wa fedha huu ambao tumeidhinishiwa na Bunge lako tukufu wa 2023/2024 kuona kama fedha ilitengwa ya kuanza ujenzi wa daraja hili. Kama fedha hiyo haikutengwa tutaangalia katika kuitenga kwenye mwaka wa fedha wa 2024/2025.