Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 481 2023-05-31

Name

Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Primary Question

MHE. NJALU D. SILANGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Nyagokolwa, Mbogo na Mhuze Wilayani Itilima?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Njalu Daudi Silanga, Mbunge wa Jimbo la Itilima, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2022/2023, TARURA iliajiri Mhandisi Mshauri ambao ni Chuo cha Ufundi Arusha kufanya uchunguzi wa kijiolojia katika Mto Garamoha ambapo kazi hiyo imekamilika kwa gharama ya shilingi milioni 35. Kwa sasa TARURA inaendelea na usanifu wa daraja hilo kwa lengo la kupata gharama halisi za utekelezaji wa ujenzi wake.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mto Isolo kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 41 kwa ajili ya kujenga daraja la mawe sehemu ya kwanza ya Mto Isolo. Ujenzi wa daraja la pili katika Mto Isolo usanifu wake utafanyika katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa kutumia wataalam wa ndani wa TARURA.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mto Mbogo, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 40 katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya usanifu wa ujenzi wa daraja kwa tekinolojia ya upinde wa mawe lenye ukubwa wa mita 15 ili kupata gharama halisi. Mto Mhuze umetengewa shilingi milioni 30 kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kijiolojia ili kuwezesha kusanifu kwa daraja hilo.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa madaraja katika Mto Garamoha, Isolo, Mbogo na Mhuze utaendelea baada ya kukamilika kwa usanifu ili kupata gharama halisi za ujenzi.