Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga wodi katika Kituo cha Afya Kihangara?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwanza ninaishukuru sana Wizara pamoja na Madaktari wote wa Wilaya ya Nyasa kwa huduma ambayo inatolewa.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza kwa kuwa hali ya kituo hiki mbali ya kukosa wodi kabisa hasa ya akina mama pia hawana ultrasound kiasi kwamba hata inapofikia kupasua mama labda kwa ajili ya mtoto mimi naona ni suala la kubahatisha, hiyo inapelekea pia kuleta changamoto.

Je, ni lini Serikali itafikiria sasa kupeleka mashine hiyo ya ultrasound ili hawa wakina mama wafanyiwe huduma iliyo kamilifu?

Swali la pili, Mheshimiwa Rais akiwa Makamu wa Rais wakati wa kampeni alipita katika Kata ya Lituhi na baada ya wananchi kumuomba akaahidi wajengewe kituo cha afya. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais ikizingatiwa kwamba ni Kiongozi Mkuu wa nchi na wananchi wanayo matumaini makubwa? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Manyanya kuhusu hali ya kituo cha afya hiki ambacho ameulizia kwenye swali lake la msingi, tutaangalia katika bajeti ambayo tunaanza kuitekeleza mwaka wa fedha 2023/2024 kuona ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa ili waweze kununua ultrasound mara moja ambayo itaenda kuhudumia akina mama wajawazito katika eneo hili la Kihangara.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la ahadi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Kata ya Lituhi kuhusu kujengewa kituo cha afya. Naomba nitumie nafasi hii kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuweza kufika katika Kata ya Lituhi na kufanya tathmini, kuona uhitaji ambao upo, idadi ya watu waliopo katika eneo hili na kisha kuwasilisha taarifa hizi katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ili katika mipango yetu tunayoweka ya ujenzi wa vituo vya afya, tuweze kuweka ujenzi wa Kituo cha Afya Lituhi ili kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga wodi katika Kituo cha Afya Kihangara?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kituo cha Afya cha Nzihi na Kituo cha Afya cha Mgama kwa kweli havina kabisa wodi za akina baba na wamekuwa wakilalamika muda mrefu na nimeshaomba mara kadhaa. Je, ni lini sasa Serikali itatujengea hizo wodi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa wodi katika Kituo cha Afya Nzihi na Kituo cha Afya Mgama kama nilivyokwishakusema kwenye majibu ya msingi, Serikali baada ya ujenzi wa vituo vya 807 sasa tunaenda kuona ni namna gani tunapata fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi kwenye vituo vya afya vilivyofanyiwa ukarabati na kupewa majengo yale ya awali yaliyoenda kujengwa katika vituo vya afya na tutaangalia pia kuhusu Kituo hichi cha Nzihi na Mgama.