Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 480 2023-05-31

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga wodi katika Kituo cha Afya Kihangara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Martin Manyanya Mbunge wa Jimbo la Nyasa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ili kuboresha huduma za afya nchini, Serikali imeanza na uboreshaji wa miundombinu ya Vituo vya Afya, kipaumbele kikiwa ni utoaji wa huduma za dharura na upasuaji ambapo fedha iliyotolewa ilielekezwa kujenga jengo la wazazi, jengo la upasuaji, jengo la maabara, jengo la kufulia na nyumba ya mtumishi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Ofisi ya Rais, (TAMISEMI) inakusudia kuanza ujenzi wa wodi za kulaza wagonjwa kwenye Vituo vya Afya ambavyo vilikwisha pokea fedha za ukarabati na ujenzi jumla ya vituo vya afya 807 vinahitaji kujengewa wodi za kulaza wagonjwa kikiwemo Kituo cha Afya Kihangara.