Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali katika kuboresha maslahi na mazingira ya kazi kwa walimu ili kuwaongezea morali ya kazi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, pamoja na jitihada kubwa za Serikali kuboresha miundombinu na kutoa vifaa, nini mpango wa Serikali sasa kutoa posho ya kufundishia (teaching allowance) kwa Walimu wote nchini ili kuongeza morali ya kazi?

Swali la pili, nini mkakati wa Serikali sasa kutoa posho ya mazingira magumu kwa watumishi hasa Walimu wanaofanya kazi kwenye mazingira magumu kijiografia kama ilivyo Ukerewe na Mafia? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza kuhusu hii posho (teaching allowance) Serikali itaendelea kuangalia suala hili na kadri ya uwezo wake wa kibajeti tutaendelea kuliona ni namna gani tunaweza tukalitekeleza. Vilevile kuna Halmashauri ambazo Wakurugenzi wao wenyewe kupitia mapato yao ya ndani wamekuwa wakitoa motisha kwa Walimu hasa wale ambao wanaenda kuripoti kwa kuwapa magodoro na vifaa vingine vya kwenda kuanzia maisha.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la posho ya mazingira magumu. Hili tunalipokea kama Serikali na tutaendelea kulifanyia analysis na kuona ni namna gani tunaweza tukapata fedha ya kuweza kulitekeleza hili lakini kwa sasa bado tutaendelea katika mazingira yote kuwa-treat watumishi wetu sawa na haki sawa katika maeneo yote.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali katika kuboresha maslahi na mazingira ya kazi kwa walimu ili kuwaongezea morali ya kazi?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi.

Mheshimiwa Spika, uhamisho pia ni sehemu ya maslahi ya walimu, je upi utaratibu ambao Serikali inautumia kwa ajili ya kuhamisha walimu kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ili waache kutufuata Wabunge tuwasaidie uhamisho?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, suala hili la uhamisho kuwa ni sehemu ya maslahi ya walimu, utaratibu uko wazi na Mwalimu anapokuwa ameajiriwa kwanza atakaa mwaka mmoja wa probation katika eneo lake ambalo amepelekwa kufanya kazi. Baada ya hapo pia atatumikia nafasi hiyo kwa miaka mingine miwili kabla ya kuomba uhamisho.

Mheshimiwa Spika, kwenye hili kumekuwa kuna influx kubwa sana ya watumishi kutaka kuhamia Mijini na kuhama maeneo ya pembezoni. Wakumbuke wakati wanaajiriwa waliajiriwa kwa sababu ya upungufu uliopo maeneo ya pembezoni ikiwemo maeneo mengine ya Halmashauri ya Wilaya ya Momba kule. Hivyo ni wajibu wao kubaki katika maeneo yale na kuhudumia Watanzania waliokuwepo kwenye maeneo yale.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali katika kuboresha maslahi na mazingira ya kazi kwa walimu ili kuwaongezea morali ya kazi?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, suala la mazingira magumu ni suala kubwa sana na kuna walimu wanaofundisha sehemu ambazo ni ngumu sana kama milimani, kuna wengine wanaishi mijini na tambarare. Serikali hamuoni kwamba ni muhimu kulichukua hili suala mara moja na kuliangalia kuliko kila wakati muwe mna repostponed na sehemu hizo ngumu zinakosa walimu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba kuna maeneo magumu ya mazingira magumu kama milimani kama Jimboni kule kwa Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, tutaendelea kuliangalia kadri ya uwezo wa kibajeti wa Serikali tutaona ni namna gani tunaweza tukaanza kufanya hivyo.