Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 37 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 479 2023-05-31

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-

Je, nini mkakati wa Serikali katika kuboresha maslahi na mazingira ya kazi kwa walimu ili kuwaongezea morali ya kazi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji kazi kwa kupeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa vituo vya mafunzo kwa walimu ambapo shilingi bilioni 1.9 zimetumika. Aidha, vitendea kazi kama vile kompyuta, printa, photocopy na projector vimenunuliwa kwa ajili ya walimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia imetoa vishikwambi kwa walimu wote wa shule za msingi na sekondari ili waendane na dunia ya sasa ya sayansi na teknolojia. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga shilingi bilioni 2.03 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya TEHAMA na taratibu za ununuzi zinaendelea. Vilevile, Serikali imetenga shilingi bilioni 5.04 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa vituo 252 vya walimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kuviimarisha vituo vya Walimu kwa ajili ya wao kukutana na kujengeana uwezo utakaowaimarisha katika shughuli za ufundishaji na ujifunzaji na itaendelea kuboresha maslahi ya Walimu kadri fedha zitakavyopatikana.