Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza kodi kwa kampuni changa?

Supplementary Question 1

MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Nachukua fursa hii kuwaombea tu kwa Mwenyezi Mungu waweze kutimiza yale ambayo wananchi wana-wish. Nina swali lingine la nyongeza: Je, utaratibu huu ambao unafanyika kwa makampuni katika kujikadiria kodi yao kwa kufanya ukokotoaji wa kile ambacho wanaingiza, ni lini utaenda kwa maduka ya kawaida ya retails? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nina ushauri kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa nini sasa kutokana na sintofahamu kubwa iliyojitokeza ndani ya nchi yetu baina ya mlipa kodi na mtoza kodi, kwa nini sasa usiwepo mfumo wa kutengeneza activities za kimichezo baina yao hata kutengeneza ligi baina ya wafanyabiashara pamoja na TRA na viwanja tunavyo pale Kariakoo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge. Kabla ya kujibu naomba nimpongeze sana kwa namna anavyojitahidi kutetea kampuni changa vile vile na wafanyabiashara wadogo wadogo. Swali lake anasema ni lini? Namwomba tu Mheshimiwa Salim awe na subira, mchakato huu unaendelea kufanywa na Serikali kwa nia safi. Mara tu baada ya kumalizika tutaleta katika Bunge lako tukufu, ahsante. (Makofi)