Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 463 2023-05-29

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza kodi kwa kampuni changa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salim Mussa Omar, Mbunge wa Jimbo la Gando kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na utaratibu wa kuzingatia misingi ya utozaji kodi, Serikali imetoa unafuu kwa biashara na kampuni changa kwa kuzitoza kodi miezi sita baada ya kuanzishwa kwake na kodi ya mapato kwa kampuni hizo huanza kutozwa baada ya kuanza kutengeneza faida ambayo hukokotolewa kulingana na faida iliyopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na zoezi la mapitio ya mfumo wa kodi ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/2024. Mwelekeo wa Serikali ni kuboresha zaidi mazingira ya kufanya biashara na kuvutia uwekezaji hasa kwa kampuni changa ikiwemo uboreshaji wa mifumo ya usimamizi wa kodi, kufanya tathmini ya tozo mbalimbali zilizopo kwa lengo la ama kupunguza viwango au kuzifuta kabisa pale ambapo zinaonekana ni kero kwa biashara au kampuni changa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.