Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y. MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je, lini Serikali itamaliza kulipa fidia kwa baadhi ya wananchi waliopisha uanzishaji wa Kambi ya Gereza la Kilimo Singa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza. Katika Wilaya ya Manyoni, tuna Gereza la Wilaya na gereza hili wanajishughulisha sana na kilimo, lakini kuna changamoto sana ya zana za kilimo za kisasa. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunaliwezesha Jeshi la Magereza la Manyoni ili waweze kujikita kwenye kilimo cha kisasa hususan kupeleka matrekta?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Katika Gereza hilo hilo la Wilaya ya Manyoni tuna upungufu mkubwa sana wa nyumba za watumishi. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba sasa tunawajengea Maafisa Magereza nyumba za kisasa ili nao wajione ni sehemu ya Tanzania? Nashukuru sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu umuhimu wa kuwa na zana za kilimo za kisasa ikiwemo matrekta, huo ndio mwelekeo mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Jeshi la Magereza kuimarisha vikosi vyake ili viweze kulima kwa tija. Kwa kufanya hivyo tumeimarisha Shirika la Uchumi la Magereza kwa maana ya SHIMA ili lianze kuzalisha kwa tija hatimaye magereza mengine ambayo hayajaingizwa katika utaratibu huu yaweze kuiga kutokana na kazi inayofanywa na SHIMA na moja ya vitendeakazi wanavyotumia ni matrekta. Kwa hiyo, Mheshimiwa atupe muda tu, tutakapokuwa tumeboresha, Gereza la Manyoni litafikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu umuhimu wa kuwa na nyumba bora za watumishi pia ni kipaumbele cha Jeshi la Magereza na kwa sasa wanatumia nguvukazi ya Jeshi la Magereza ili kujiimarisha kwa kujenga nyumba zinazofaa. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kumwomba Mkuu wa Magereza Mkoa wa Singida awasiliane na wenzie wa Magereza yake ndani ya mkoa waanze miradi ya kujenga nyumba za maafisa ili Serikali kwa maana ya Magereza Makao Makuu yaweze kuwa–support vifaa vya kukamilishia majengo hayo, nashukuru. (Makofi)