Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 462 2023-05-29

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y. MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itamaliza kulipa fidia kwa baadhi ya wananchi waliopisha uanzishaji wa Kambi ya Gereza la Kilimo Singa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi Singa ilianzishwa mwaka 1983 katika Kijiji cha Singa chini ya Magereza ya Mkoa wa Singida ikiwa na eneo la ekari 500 kama ilivyoombwa kutoka Serikali ya Kijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Ardhi (Land Ordinance 03, Cap 113) ya mwaka 1923 iliyokoma mwaka 2003 haikuruhusu ulipwaji wa fidia kwa maeneo yanayotwaliwa na Serikali ambayo hayajaendelezwa. Kwa kuzingatia sheria hiyo, wananchi walio na maeneo yaliyoendelezwa (kwa kupanda mazao ya kudumu) katika eneo lililogawiwa kwa gereza walilipwa fidia zao shilingi 300,000 kwa eneo lenye ukubwa wa ekari 10 na malipo ya mwisho yalifanyika mwaka 1997. Taratibu za umilikishaji rasmi wa eneo hilo kwa Jeshi la Magereza zinakamilishwa na Mamlaka husika, nashukuru.