Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani hadi Mziha kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kwenye swali hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inaunganisha Mkoa wa Tanga na Mkoa wa Morogoro pia imekuwepo kwenye Ilani za Uchaguzi za CCM tangu enzi za Mzee Mkapa, Mzee Kikwete, Hayati Magufuli na sasa Rais Samia. Je, kwa nini Serikali isiweke Wakandarasi Mwaka wa Fedha 2023/2024 kwa barabara nzima kilometa 104 yaani Turiani – Mziha – Handeni badala ya kuweka kipande hicho kidogo? (Makofi)

Swali la pili la nyongeza, kwenye bajeti za Wizara hii kwa mwaka wa fedha 2020/2021, 2021/2022, 2022/2023 na sasa 2023/2024 barabara hii imekuwa ikitengewa kiasi hiki cha fedha cha bilioni moja na majibu ya Serikali yamekuwa ni haya haya.

Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mkoa wa Tanga na Mkoa wa Morogoro kuhusu barabara hii na ahadi zake zisizotekelezeka? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara aliyoitaja ipo kwenye Ilani na ni kweli kwamba inaunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Tanga, ni barabara ambayo kwa kweli ina historia yake na kwa maana hiyo Serikali ilishaanza kuijenga hadi Turiani, kwa sasa Serikali imedhamiria kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kuanzia Turiani, Mziha hadi Handeni, Kilometa 104, lakini kuweka Wakandarasi zaidi ya mmoja utaharakisha lakini kutategemea sana na upatikani wa fedha ili kuweza kuweka Wakandarasi zaidi ya mmoja kwa kipindi kimoja. Dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwamba kwa mwaka ujao wa fedha tunaendelea pale tulipoishia kukamilisha barabara hii hadi Handeni. Ahsante. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani hadi Mziha kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona.

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa barabara ya Katoma hadi Bukoli kwa kiwango cha lami ndani ya Wilaya ya Misenyi, Mkoani Kagera?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Semuguruka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Katoma kwenda Bukoli ipo inaendelea kujengwa lakini kwa awamu. Mwaka huu wa fedha imetengewa pia fedha ambapo tunategemea kwamba tutajenga zaidi ya kile tulichokuwa tunakijenga ili kuikamilisha barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani hadi Mziha kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itasaini mkataba wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, barabara kuanzia Kongwa – Kiteto – Simanjiro hadi Arusha na Tanga – Kiteto hadi Singida? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye bajeti tulitaja barabara aliyoitaja Kongwa - Kibaya – Orkesumet - Losinyai hadi Arusha ambayo tunachosubiri sasa ni baada tu ya Bunge hili sasa ambalo tunategemea kabla ya Mwezi Juni barabara hiyo iwe imesainiwa kwa mpango wa EPC + F. Ahsante. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani hadi Mziha kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Masasi – Nachingwea - Liwale itajengwa kwa utaratibu wa EPC + F tuliambiwa Mkandarasi amepatikana. Ni lini mkataba utatiwa saini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kama nilivyojibu katika swali ambalo nimeulizwa barabara hizi ziko saba na moja ya barabara hiyo ni ya Masasi – Nachingwea hadi Liwale. Mikataba ilishakamilika kinachosubiriwa ni muda na kwa sasa kwa sababu ni miradi mikubwa signing itafanyika muda wowote iko tayari kwa ajili ya signing na tunategemea kabla ya mwisho wa mwezi Juni barabara hii ya Masasi – Liwale – Nachingwea kilometa 175 itakuwa imesainiwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani hadi Mziha kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Barabara ya Utegi – Shirati mpaka Kirongwe kwa kuwa upembuzi yakinifu umekwishakamilika na barabara imeingizwa kwenye bajeti. Nataka nijue nini mpango wa Serikali sasa kuanza ujenzi wa barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ndiyo imetengewa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, tunajua upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishakamilika, kwa hiyo taratibu za manunuzi kuanza ujenzi wa barabara hiyo zitaanza mwaka wa fedha wa 2023/2024 kama ilivyopitishwa na Bunge hili kwa maana ya mwaka ujao wa fedha. Ahsante.