Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 461 2023-05-29

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Turiani hadi Mziha kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Turiani hadi Mziha, yenye urefu wa kilometa 35.5 kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami imekamilika. Serikali imepanga kujenga ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa awamu katika mwaka wa fedha 2023/2024. Ahsante.