Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaweka wazi mikataba ya sekta ya uziduaji kama The Extractive Industries Transparency Initiative inavyotutaka?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tunayo Sheria Tanzania Extractive Industry Transparency Initiative Act ya mwaka 2016, Section Number 16 ambayo inataka mikataba yote ya Sekta ya Uziduaji iwekwe wazi na iwekwe wazi kwenye website pamoja na vyombo vya habari media zote Tanzania. Nataka kujua commitment ya Serikali, kwa sababu EITI wanakuja validation Tanzania mwaka huu.

Serikali imejipangaje kuhakikisha kwamba mnalinda reputation ya nchi kwa kuwa na sheria ambayo haitekelezeki kwa muda mrefu toka 2016? (Makofi)

Swali la pili, nataka commitment ya Serikali ni lini suala hili linakwenda kukamilika kwa sababu limekaa kwa muda mrefu sana? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimjibu Mheshimiwa Jesca Kishoa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali lake la kwanza, Wizara yetu ya Madini na wakifanya kazi pamoja na TEITI na mamlaka nyingine ya Serikali ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wako katika mchakato ambao unachambua na kufanya kazi kwa kushirikiana na kampuni zote zilizowekeza katika sekta za rasilimali hizi ili kuona namna bora ya kuweka wazi hiyo mikataba kwa mujibu wa matakwa ya Sheria ya Taasisi ya Kimataifa ya EITI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kwamba ni lini? Kwa ratiba tuliyonayo tunategemea kwamba kufika Mwezi wa Kumi mwaka huu taratibu zote zitakuwa zimekamilika na hivyo mikataba hiyo itakuja kuwekwa wazi kwa mujibu wa matakwa ya Taasisi ya Kimataifa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaweka wazi mikataba ya sekta ya uziduaji kama The Extractive Industries Transparency Initiative inavyotutaka?

Supplementary Question 2

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Kwa kuwa, Serikali imeendelea kukaidi na kukiuka sheria katika uingiaji na usimamizi wa mikataba ya uziduaji ambayo ni madini gesi na mafuta na pamoja na matakwa yale ya TEITI lakini pia kuna matakwa ya Sheria Kifungu 12 cha (The Natural Wealth and Resources (Permanent Sovereignty) No. (5) Act, 2017) ambayo…

MWENYEKITI: Mheshimiwa swali.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ambayo inataka mikataba yote iletwe hapa Bungeni. Kwa nini Serikali inaendelea kukiuka matakwa haya ya kisheria? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali haina mpango wala haifanyi maksudi kwamba lazima sheria iliyowekwa ikiukwe. Sheria zote zinasimamiwa na Serikali na Wabunge wote nasi Watendaji wote wa Serikali tumeapa kusimamia sheria ya nchi na Katiba ya nchi, kwa hivyo kama kuna ambayo haitekelezwi ni suala lingine la kuangalia tu mikakati ya Serikali ya kujisimamia na kuhakikisha kwamba sheria zinatekelezwa kwa mujibu wa jinsi zilivyotungwa lakini hakuna utaratibu wowote wa kwamba Serikali inakusudia na inavunja sheria yeyote.