Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Energy and Minerals Wizara ya Madini 460 2023-05-29

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaweka wazi mikataba ya sekta ya uziduaji kama The Extractive Industries Transparency Initiative inavyotutaka?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni mwanachama wa Asasi ya Kimataifa ya EITI (Extractive Industries Transparency Initiative). Ambalo jukumu lake kuu ni kuhamasisha Serikali kuweka mifumo ya uwazi katika rasilimali madini, mafuta na gesi asilia ili kuboresha mapato na manufaa yanayotokana na shughuli za utafutaji na uchimbaji wa rasilimali hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza takwa la uwekaji wazi wa mikataba Taasisi ya TEITI imeandaa Mpango kazi (Roadmap) kwa ajili ya utekelezaji wa kazi ya uwekaji wazi mikataba. Mpango huo umewekwa wazi kwa ajili ya utekelezaji kulingana na matwaka ya Kimataifa ya Taasisi ya EITI. Kwa hivyo, katika mwaka wa fedha 2023/2024 TEITI imeweka mkakati wa kuhakikisha kuwa mikataba inawekwa wazi, ikiwa ni pamoja na kushauriana na mamlaka nyingine za Serikali namna bora ya kutekeleza mikataba na takwa hili. Ahsante.