Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kuzungumza na wenye viwanda vya mbolea ili kuwe na ujazo wa kilo tofauti na 50?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Sswali la kwanza, kama ni hivyo ni kwa nini sasa mbolea hizo kwa vifungashio ulivyovitaja hazipo madukani? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa mvua za kwanza ni za kupandia. Je, katika Mkoa wa Kigoma kwa mwaka huu mbolea zitafika Mkoa wa Kigoma mwezi gani? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema mbolea hizi za ujazo tofauti tofauti hutokana na mahitaji halisi ya maeneo husika na aina ya mazao yanayolimwa. Kwa sababu imeonekana kuna mahitaji hayo, kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Ubora wa Mbolea Tanzania - TFRA tutatoa maelekezo kwa wazalishaji na waingizaji wa mbolea hapa nchini kuhakikisha kwamba wanatoa mbolea kulingana na mahitaji na hasa katika hoja ambayo Mheshimiwa Mbunge ameisema ya kuanzia kilo tano, 20, mpaka 10 na kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu mbolea kufika lini. Tulishasema ndani ya Bunge lako Tukufu ya kwamba tunataka tuhakikishe changamoto za msimu uliopita safari hii zisijirudie na mbolea ifike nchini kwa wakati, wakati wakulima wetu wakiwa bado wana nguvu ya kuweza kununua hasa baada ya kuwa wametoka kuuza mazao yao. Ni commitment ya Serikali kwamba tutahakikisha ndani ya mwezi wa Saba mbolea imefika hapa nchini na wakulima waanze kununua kwa ajili ya msimu ujao. (Makofi)