Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 459 2023-05-29

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Je, Serikali ipo tayari kuzungumza na wenye viwanda vya mbolea ili kuwe na ujazo wa kilo tofauti na 50?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyeketi, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 32, (4) na (5) pamoja na Kanuni ya 33(1) ya Kanuni za Mbolea za mwaka 2011, wazalishaji au waingizaji wa mbolea wanaruhusiwa kufungasha mbolea katika ujazo unaofaa kwa watumiaji mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbolea zilizo katika hali ya yabisi (solid fertilizers) zinapaswa kufungashwa katika ujazo wa kilo tano, 10, 25 na 50. Mbolea zilizo katika hali ya kimiminika (liquid fertilizers) zinapaswa kuwa katika ujazo wa mililita tano, 10, 20, 50 na 100. Aidha, visaidizi vingine vya mbolea kama vile chokaa mazao (agricultural lime) na jasi (gypsum) hufungashwa katika ujazo wa kilo tano, 10, 20, 50 na 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kusimamia wazalishaji wa mbolea kuzalisha mbolea kulingana na mahitaji.