Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya bei ndogo za mazao pamoja na ukosefu wa masoko ya uhakika nchini?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimshukuru waziri kwa majibu yake mazuri sana aliyoyatoa hapa hivi sasa, lakini nina maswali yangu mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa suala hili ni la muda mrefu, je, Serikali inaweza kutuambia nini hali halisi kwa sasa pamoja na mifano?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kwa kuwa ongezeko la thamani, mazao yetu hapa nchi kuna maboresho ya mazao yetu, je, Serikali iko tayari kutengeneza viwanda vidogovidogo katika wilaya zetu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hali halisi ya upatikanaji wa masoko ya mazao yetu. Nataka nikiri mbele ya Bunge lako kwamba hivi sasa katika baadhi ya mazao hasa mazao ya nafaka soko la mazao haya limekuwa ni kubwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania na hivyo kuwawezesha wakulima wetu wengi kuwa na masoko ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hivyo katika matunda na mbogamboga pia na kwenyewe tunafanya vizuri hivi sasa parachichi letu limepata nafasi ya kwenda katika masoko ya Hispania, China, Marekani, pamoja na Afrika ya Kusini hii ni ishara njema kuonesha kwamba kuna kazi imefanyika kwenye kutangaza mazao yetu, lakini pia kwenye kahawa na korosho na mazao mengine pia tunafanya vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuongeza thamani, ni mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunaendelea kuongeza thamani ya mazao yetu ya kilimo. Mkakati uliopo hivi sasa ni kuhakikisha kwamba tunajenga uwezo kwa uanzishaji wa viwanda vidogovidogo kuanzia kule katika eneo la korosho na mazao mengine ya nafaka. Hivi sasa bodi ya mazao mchanganyiko yenyewe tu imeshaendelea kuwekeza katika vinu vingi vya kusaga mazao ya nafaka ili kuongeza thamani ya mazao yetu. Hii ni hatua ya Serikali lakini pia na sekta binafsi wanatuunga mkono.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya bei ndogo za mazao pamoja na ukosefu wa masoko ya uhakika nchini?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Nataka kujua kauli ya Serikali kuhusu kuporomoka kwa zaidi ya asilimia 50 kwa bei ya alizeti kwa wakulima na hali nchi ina upungufu mkubwa wa kujitosheleza katika uzalishaji wa mafuta ya kula?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli bei ya alizeti imeporomoka na imesababisha kuwakatisha tamaa wakulima, lakini sisi Wizara ya Kilimo pamoja na Wizara ya Fedha tumekaa chini na kuangalia namna bora ya kuweza kutatua changamoto hii ikiwemo kuangalia sera zetu za fedha na hasa katika kuliboresha eneo la kuongeza kodi kwa mafuta ambayo yanaagizwa kutoka nje ya nchi ili kuweza kuwalinda wakulima wetu wa ndani. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya bei ndogo za mazao pamoja na ukosefu wa masoko ya uhakika nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa asilimia 72 ya zao la tangawizi inalimwa ndani ya Jimbo la Same Mashariki na kwa kuwa bei ya zao hili kwa wananchi bado siyo rafiki kabisa. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri aniambie watatumia mkakati gani wa kuwafanya hawa wananchi wapate bei ambayo itawatia moyo wa kuendelea kulima zao hili muhimu nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua kwamba tunao wajibu kama Serikali kuhakikisha kwamba wakulima wanapata bei bora ya mazao yao, Serikali imeanzisha mamlaka maalum ambayo inaitwa COPRA kwa ajili ya usimamizi wa masoko na bei ya wakulima ikiwemo wakulima wa tangawizi. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutahakikisha tunashirikiana sisi na yeye ili wakulima wake waweze kupata bei bora na kilimo kiweze kuimarika katika eneo lake hilo la Same.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya bei ndogo za mazao pamoja na ukosefu wa masoko ya uhakika nchini?

Supplementary Question 4

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri, Chuo cha TARI Naliendele zaidi ya miaka 20 sasa wamekamilisha utafiti unaoonesha kwamba kutokana na nipa inayopatikana kwenye korosho ina uwezo wa kuzalisha ethanol methanol pamoja na alcohol kwa matumizi ya burudani pamoja na hospitali, lakini pia kuongezea kipato wakulima na kupunguzia Taifa hili hasara. Je nini mkakati wa Serikali kuhakikisha sasa nipa inakuwa rasmi kwa ajili ya kupunguzia hasara Taifa letu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesikia hoja ya Mbunge, tutaishirikisha TARI pamoja na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ili ikibainika kwamba nipa hiyo inaweza ikatumika katika maeneo ambayo ameyataja, basi sisi kama Serikali kwa kushirikiana na TARI tutasaidia kuongeza mnyororo wa thamani wa zao la korosho.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya bei ndogo za mazao pamoja na ukosefu wa masoko ya uhakika nchini?

Supplementary Question 5

MHE EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kuwa wakulima walihamasika sana kuhusu alizeti na bei imeteremka na wakati wanaangalia sheria ili wazuie mafuta yanayotoka nje, kwa nini Serikali isifanye commitment au kununua alizeti yote ambayo wakulima wamelima?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumepata changamoto ya bei kuporomoka na ndiyo maana kwenye bajeti yetu Mheshimiwa Waziri alitamka kwenye kitabu chake cha bajeti uanzishwaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo (ADF) Agricultural Development Fund ambayo kazi yake nyingine ni kwa ajili ya price stabilization.

Mheshimiwa Mwenyekiti, habari njema ni kwamba tumeshapata amri kutoka Wizara ya Fedha ya uanzishwaji wa Mfuko huu na Mfuko utaanza kufanya kazi, natumai katika changamoto ambazo zitajitokeza baadaye basi Serikali kupitia Mfuko huu inaweza kufanya kazi hiyo kwa ajili ya kuwa rescue wakulima. (Makofi)