Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 457 2023-05-29

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya bei ndogo za mazao pamoja na ukosefu wa masoko ya uhakika nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha wakulima wanapata bei shindani na masoko ya uhakika. Mikakati hiyo ni pamoja na kuongeza tija kwenye uzalishaji kupitia uwekezaji katika miundombinu ya umwagiliaji, pembejeo, utafiti, huduma za ugani, matumizi ya teknolojia na kurasimisha Sekta ya Kilimo Mazao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Serikali inaendelea kuhamasisha kilimo cha kibiashara kinachozingatia mahitaji ya soko; kushiriki makongamano na maonesho ya kibiashara na uwekezaji kwa lengo la kutangaza bidhaa na maeneo ya uwekezaji katika sekta ya kilimo; kushirikiana na Sekta Binafsi katika ujenzi wa miundombinu ya masoko; kuimarisha mifumo ya kielektroniki ambayo itawezesha upatikanaji wa taarifa za masoko kwa wakati; kutoa mafunzo kuhusu kilimo biashara kwa Maafisa Ugani na Wakulima na kuendelea kufungua masoko mapya katika nchi mbalimbali kwa kufanya tafiti za mahitaji kwa nchi husika.