Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza:- Je, kuna mkakati gani wa kutoa mafunzo ya kuogelea kwa wakulima wa Mwani Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA SALUM MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imekiri kabisa kwamba asilimia kubwa ya wakulima wa zao hili ni wanawake, je, mkakati wa kutoa elimu pia kuwahusisha wanaume ili na wao waweze kujiongezea kipato kupitia zao hili ukoje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa product itokanayo na zao la mwani ni muhimu sana kwa afya ya wananchi wote wakiwemo wanaume pamoja na wanawake. Je Serikali haioni haja sasa ya kutumia Vyombo vya Habari kuujulisha umma umuhimu wa zao hili ili wananchi wengi waweze kulilima na kupata mazao au kupata ajira zitokanazo na zao hili? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kutambua umuhimu wa zao hili na jitihada mojawapo ya sasa na mkakati ambao tulionao katika maeneo ambayo yanazunguka Ukanda wa Pwani na wamekuwa wakituona maeneo mbalimbali ni kutangaza kwa makundi yote mawili wanawake na wanaume kuhakikisha wanashiriki katika zao hili la mwani. Kwa hiyo kazi hiyo tunaifanya na tutaongeza jitihada kuifanya ili ongezeko la watu wanaojihusisha na shughuli hizo wawe wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kutumia Vyombo vya Habari, sasa hivi tumekuwa tukifanya ukiangalia TBC kuna vipindi vinavyohusisha kilimo cha mwani, lakini tutaongeza mara dufu zaidi ili tutanue wigo mpana ili vyombo vya Habari viweze kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo jambo hilo tumelipokea na tutalifanya, ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza:- Je, kuna mkakati gani wa kutoa mafunzo ya kuogelea kwa wakulima wa Mwani Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Kigamboni ina ukanda wa bahari takribani kilomita 70, nataka kujua nini mkakati wa Serikali wa kukuza kilimo cha mwani na jongoo bahari katika Wilaya ya Kigamboni kama mkakati wa kuchochea uchumi wa bluu na kuongeza ajira nchini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwondoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya mkakati wetu mkubwa ni kuhakikisha tunafikia maeneo yote ya ukanda wa pwani na ndio maana hivi karibuni tumepata fedha kutoka maeneo mbalimbali. Juzi tumesaini mkataba wa fedha karibu dola milioni 13 na watu wa USAID na sehemu ya hizo fedha ni pamoja na kuhamasisha kilimo cha mwani na majongoo bahari katika Ukanda wa Pwani ikiwemo Kigamboni. tumefanya hivyo Ifani, Tanga, kwa hiyo ni jambo ambalo lipo katika mchakato. Ahsante.