Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 456 2023-05-29

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA K.n.y. MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kutoa mafunzo ya kuogelea kwa wakulima wa Mwani Zanzibar?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asya Sharif Omar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa zao la mwani katika kuongeza kipato, ajira na kukuza uchumi katika ukanda wa pwani na Taifa kwa ujumla. Vilevile, inatambua kuwa, zaidi ya asilimia 90 ya wakulima wa mwani ni wanawake. Ili kuwa na kilimo endelevu na kulinda usalama wa wakulima wa mwani wawapo katika shughuli zao, ni muhimu wakulima hawa kuwa na ujuzi wa kuogelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimekuwa na mikakati mbalimbali kuhakikisha wakulima wa mwani wanapatiwa nyenzo bora za kuhakikisha usalama mahali pa kazi. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zitatoa mafunzo ya kuogelea kwa wakulima wa mwani pamoja na kununua na kusambaza vifaa vya kulinda usalama wakiwa kwenye maji wakishughulika na kilimo cha mwani.