Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Kata ya Kasanga itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba nipongeze majibu mazuri ya Serikali. Lakini pamoja na pongezi hiyo naomba niulize maswali madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhitaji wa vituo vya afya kwa ajili ya kutoa huduma za afya unahitajika sana katika Wilaya ya Kalambo na Halmashauri ya Kalambo na wananchi kwa kulijua hilo wameweza kujenga zahanati nane na ziko usawa wa lintel. Zahanati hizo ni pamoja na Uyumi, Sengakalonje, Limba, just to mention. Je, Serikli haioni kwamba iko sababu ya kuhakikisha kwamba inapeleka fedha ili kumalizia juhudi kubwa zilizofanywa na wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, uhitaji wa kujenga kituo cha afya katika Kata ya Katete ni wa muhimu sana kwa kuzingatia jiografia yake; Je, Serikali haioni kwamba iko sababu ya kuhakikisha kwamba katika bajeti inayokuja maeneo haya yanapelekewa fedha ili vituo vya afya vijengwe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kandege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza juu ya hizi zahanati ambazo zimejengwa kwa jitihada za wananchi wa kule Kalambo. Kwanza nitoe pongezi tena kwa wananchi wa kule Kalambo kwa jitihada zao za kujenga maboma haya ya zahanati, lakini vile vile niseme mbele ya Bunge lako tukufu kwamba ni azma ya Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha ina boresha afya za Watanzania kwa kujenga zahanati na vituo vya afya, hospitali za wilaya na hospitali za mikoa na rufaa kadri ya upatikanaji wa fedha. Hivyo basi sisi kama Serikali tutaangalia zahanati hizi na kuona ni namna gani tunaweza tuka-support katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 katika umaliziaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda katika swali lake la pili la kujenga Kituo cha Afya cha Katete. Tutatuma timu kule Kalambo kwenda kufanya tathmini ya Kituo hiki cha Afya cha Katete, na tutaona ni namna gani tunaweza tuka-support jitihada hizi ambazo Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa kule Kalambo wote wamezifanya, za kupata kituo cha afya hapa. Mara tu tathmini itakapokamilika basi tutaona ni namna gani tunatenga fedha katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Kata ya Kasanga itatekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Kwa kuwa nilishaomba Kata ya Mgombasi tunashida ya kuwa na kituo cha afya ilhali ni kata ambayo ina watu wengi sana.

Je, Serikali iko tayari kutuambia ni lini au iko katika mpango wa bajeti hii kujenga kituo cha afya kata ya Mgombasi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotoka kujibu swali la Mheshimiwa Kandege la kutuma timu kufanya tathmini ya kuona wingi wa watu na uhitaji wa kituo cha afya, basi pia nichukue nafasi hii kusema kwamba timu hii tutahakikisha pia inafika kwa Mheshimiwa Kawawa kule katika kata ya Mgombasi na kufanya tathmini na kuona idadi ya watu waliokuwa pale na uhitaji uliopo ili Serikali iweze kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho cha afya.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Kata ya Kasanga itatekelezwa?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kata za Kia, Muungano, Uroki, Mnadani na Weruweru ni kata ambazo hazina vituo vya afya na wananchi wanatembea umbali mrefu sana kwenda kufata huduma kule Bomang’ombe.

Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya kwenye kata hizi muhimu sana?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itajenga vituo vya afya hivi muhimu katika Kata za Kia, Muungano, Uroki katika halmashauri ya Wilaya ya Hai kadri ya upatikanaji wa fedha. Lakini vile vile nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kuweza kufanya tathmini ya zahanati hizi zilizoko katika kata alizozitaja Mheshimiwa Saashisha ili kuona ni namna gani zinakidhi vigezo vya kupandishwa hadhi na kuwa vituo vya afya ndipo tuweze kuona ni namna gani tunatenga fedha katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Kata ya Kasanga itatekelezwa?

Supplementary Question 4

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa juhudi kubwa za Serikali zimefanyika kujenga hospitali vituo vya afya vya kileo;

Je, Serikali ina mpango gani kuhimarisha huduma ya kinywa na meno katika vituo vya afya na zahanati zote nchini, kwa sababu sehemu hiyo inaonekana kusahaulika?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha inaboresha afya za Watanzania ikiwemo afya ya kinywa na meno. Na ndio maana Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imetenga fedha nyingi sana katika ununuzi wa vifaa tiba vikiwemo hivi vya kinywa na meno. Tayari tuna timu ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ambayo inazunguka kwenye maeneo yote yaliyopatiwa vifaa tiba kutoa mafunzo kwa wataalam wetu kuona ni namna gani wanaweza kuanza kutumia vifaa hivi kutoa huduma ya kinywa na meno kwenye hospitali zetu za wilaya na kwenye vituo vyetu vya afya vya kimkakati.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Kata ya Kasanga itatekelezwa?

Supplementary Question 5

MHE AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kituo cha Afya Kabwe kikikamilika kinategemea kuhudumia zaidi ya kata tatu. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka fedha ili kumalizia kituo hiki kifanye kazi katika hizo kata tatu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka fedha katika Jimbo la Nkasi kwa Mheshimiwa Aida kule kwa ajili ya kujenga kituo cha afya ambacho amekitaja kadri ya upatikanaji wa fedha. Vilevile nitumie nafasi hii kusema tutatuma timu ambayo nimeisema pia itaelekea kule Kalambo kwa sababu ni mkoa mmoja timu hii pia iweze kufika katika kituo hiki cha afya na kufanya tathmini na kuona ni namna gani tunaweza tukatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki cha afya.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya kujenga Kituo cha Afya Kata ya Kasanga itatekelezwa?

Supplementary Question 6

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu alipofanya ziara kwenye Wilaya ya Chemba kwenye Kijiji cha Itwalo aliahidi Serikali kujenga kituo cha afya, lakini hivyo hivyo kwenye Kata ya Tarangi. Naomba kujua ni lini utekelezaji wa ujenzi huu utafanyika? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni kwanza nilitaarifu Bunge lako kwamba, Serikali inatoa kipaumbele cha kukamilisha ahadi zote za Viongozi wetu wa Kitaifa kuanzia Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi tutaangalia katika kata hizi mbili ambazo Mheshimiwa Monni amezitaja ni namna gani tunaweza tukatenga fedha ama kama imetengewa fedha kwenye mwaka huu wa fedha unaoenda kuanza wa 2023/2024, tuweze kuanza ujenzi huu mara moja na kama fedha haijatengwa, basi tutenge fedha kwenye mwaka wa fedha wa 2024/2025.