Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Vituo vya Afya vya zamani ikiwa ni pamoja na kujenga Chumba cha kuhifadhi Maiti?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hali iliyoko Kalenga ni sawa sawa na hali iliyoko Busanda tunavyo vituo viwili vya Chikobe na Bukori. Nini mkakati wa Serikali wa kuviboresha vituo hivyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali lake la nyongeza la lini Serikali itatenga fedha za katika Vituo vya Afya vya Chikobe na Bukoli. Ni lengo la Serikali kuhakikisha inajenga vituo vya afya vya kimkakati kote nchini; na ndiyo maana katika mwaka wa fedha huu ambao unamalizika tarehe 30 Juni mwaka huu Serikali ilitenga bilioni 117 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati kote nchini. Hivyo basi tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi huo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pale ambapo fedha zitapatikana tutavitenga vituo hivi vya afya vya Chikobe na Bukoli.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Vituo vya Afya vya zamani ikiwa ni pamoja na kujenga Chumba cha kuhifadhi Maiti?

Supplementary Question 2

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kituo cha Afya cha Kiloreli kilipandishwa hadhi, kutoka zahanati na baadaye kikawa kituo cha afya, lakini bado hakina majengo yoyote yenye kukidhi kuwa kituo cha afya;

Je, Serikali ina mpango wowote kuleta fedha kwa ajili ya kuongeza majengo pale?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba inajenga majengo yote ambayo yanahitajika kwenye vituo vya afya hapa nchini, kikiwemo ambacho amekitaja Mheshimiwa Songe cha kule Wilayani Busega. Hivyo basi kadri ya upatikanaji wa fedha tutahakikisha tunapeleka fedha katika kituo hiki cha afya ili kiweze kuapata majengo yanayohitajika.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Vituo vya Afya vya zamani ikiwa ni pamoja na kujenga Chumba cha kuhifadhi Maiti?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa Bunda Mjini katika Kata ya Manyamanyama walianza ujenzi wa nyumba mbili za watumishi kwa nguvu zao;

Je, ni lini Serikali sasa mtakamilisha maboma hayo ya nyumba za watumishi ambayo yamekaa kwa muda mrefu kwenye Hospitali ya Manyamanyama?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kuwapongeza sana wananchi wa Bunda Mjini na wa Kata hii ya Manyamanyama kwa kuweza kujitoa na kuanza ujenzi wa majengo ya nyumba za watumishi. Serikali itafanya tathmini ya majengo hayo kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Mjini, na pale tathmini itakapokamilika tutaona ni namna gani tunatenga fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025.