Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 453 2023-05-29

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA K.n.y. MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuimarisha Vituo vya Afya vya zamani ikiwa ni pamoja na kujenga Chumba cha kuhifadhi Maiti?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za afya. Tayari Ofisi ya Rais TAMISEMI, imekwishakusanya orodha ya vituo vya afya vinavyohitaji ukarabati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Rais TAMISEMI, ilipoanza kusimamia mpango maalum wa kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya ya msingi mwezi Oktoba 2023, jumla ya vituo vya afya 379 kati ya vituo vya afya 697 vimekarabatiwa na kuongezewa miundombinu iliyopungua ikiwemo wodi za uzazi, vyumba vya upasuaji na majengo ya kuhifadhia maiti. Jumla ya majengo 117 ya kuhifadhia maiti yamejengwa na kuwekewa majokofu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepanga kukarabati vituo vya afya 50 kupitia fedha za Mfuko wa Afya wa Dunia, ili kuviwezesha vituo hivyo kutoa huduma za dharura na upasuaji kwa mama mjamzito. Serikali, itaendelea kutoa fedha kwa ajili ya kukarabati vituo vya afya ili kuviwezesha kutoa huduma zinazokosekana likiwemo jimbo la Kalenga.