Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Stendi ya Mabasi yaendayo Mikoa ya Kusini katika eneo la Mbagala?

Supplementary Question 1

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali langu la kwanza; kwa kuwa fedha za ujenzi zilitengwa tangu 2023/2024 na kwa kuwa eneo hakuna;

Je, ni kwa nini hizo fedha zisitumike sasa kufidia eneo la kujenga stendi hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kutokana na umuhimu wa stendi hiyo juu ya Serikali pamoja na wananchi wa Temeke;

Je, haioni sasa kuna umuhimu wa kuwa na sababu ya kuipa fedha za miradi ya mikakati Halmashauri yetu ya Temeke ili kuendeleza ujenzi huu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Chaurembo; la kwanza, hili la mwaka wa fedha 2024/2025 hii ni fedha ambayo wameitenga. Kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, fedha hii bilioni mbili imetengwa katika mwaka wa fedha tunaoenda kuanza, yaani July mwaka 2023/2024 sasa ni maamuzi yao wenyewe kupitia kikao chao cha finance na maamuzi ya halmashauri, kama wataweza kufanya fidia kutokana na fedha hii wanaweza wakalipa ili wa-secure ili lile eneo liwe ni la kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili, umuhimu wa Serikali kuipa fedha, Halmashauri ya Manispaa ya Temeke. Tunatambua kwamba ni jambo la muhimu sana kuwa na maeneo ya miradi ya kimkakati hapa nchini ili kuziwezesha halmashauri zetu kuongeza uwezo wa kipato. Tutawapatia fedha wakiandika andiko na kulileta Ofisi ya Rais TAMISEMI na kisha sisi kulichakata na kulipeleka katika Wizara ya Fedha ambapo ndio wanaotoa fedha hizi. Kwa hiyo niwaatoe hofu wana Temeke na wana Mbagala kwamba pale tutakapo pokea andiko lao basi tutatenga fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa stendi hii.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Stendi ya Mabasi yaendayo Mikoa ya Kusini katika eneo la Mbagala?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakazi wa Mkoa wa Kagera wamekuwa wakipata adha kwa kukosa stendi ambayo iko ndani ya Manispaa ya Bukoba, ambayo Mbunge wa Jimbo ndugu yangu Steven Byabato amekuwa akifatilia.

Je, ni lini sasa Stendi hiyo itajengwa ili kuweza kusaidia wananchi wa Mkoa wa Kagera?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kyombo kuhusu stendi ya Manispaa ya Bukoba. Serikali itapeleka fedha hizo pale maandiko haya yatakuwa yamepitiwa na kuona sustainability.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni miradi ya kimkakati, na kwa kuwa ni ya kimkakati lazima ioneshe sustainability, kwamba watakapopatiwa fedha na kujenga miradi hii basi halmashauri itaweza kuingiza mapato ya kujiendesha. Kwa hiyo pale ambapo tutamaliza mchakato wa ku-review andiko hili lililoletwa na Manispaa ya Bukoba tutawasilisha Wizara ya Fedha ili nao waweze kutenga fedha kwa ajili ya stendi hii.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Stendi ya Mabasi yaendayo Mikoa ya Kusini katika eneo la Mbagala?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi niweze kuulizwa swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halmashauri ya Wilaya ya Karatu pia ina mpango wa kujenga stendi ya kisasa, na kwenye bajeti ijayo, halmashauri umetenga fedha kidogo, tunajua haitaweza kutosheleza.

Je, Serikali kuu iko tayari sasa ku top-up hicho kidogo kilichotengwa na halmashauri ili malengo yaweze kufikiwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Paresso la Stendi ya Karatu. Kwanza ni pongeze jitihada za halmashauri ya Karatu kwa kutenga fedha zao kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa stendi hii. Ni dhamira ya Serikali hasa hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha inawezesha halmashauri zetu zote nchini kuwa na uwezo wa kupata mapato, kama nilivyosema awali, ambayo ni sustainable kwa ajili ya uendeshaji wa halmashauri hizi. Hivyo tutakapo pokea andiko kutoka Halmashuri ya Karatu juu ya ujenzi wa stendi hii basi tutaangalia tutachakata andiko hilo na kuliwasilisha Wizara ya Fedha.