Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 452 2023-05-29

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Stendi ya Mabasi yaendayo Mikoa ya Kusini katika eneo la Mbagala?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Jimbo la Mbagala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na stendi ya mabasi yaendayo kusini katika eneo la Mbagala. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imetenga kiasi cha shilingi bilioni mbili kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Temeke inaendelea na taratibu za kupata eneo la kujenga stendi hiyo katika Kata ya Mbagala. Pindi eneo litakapopatikana ujenzi utaanza.