Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha Wilayani Ludewa hususan eneo la elimu, afya na uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, hata hivyo, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni kawaida ya Serikali kuwapangia watumishi Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa na kuwahamisha kabla hawajaripoti hasa madaktari, je, nini mpango wa Serikali kutoa ajira mbadala kwa nafasi hizo ambazo madaktari hawakuripoti?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kumekuwa na changamoto ya wananchi kulazimika kuajiri walinzi kwa ajili ya kulinda shule za sekondari na zahanati, je, nini mkakati wa Serikali kuajiri walinzi hawa ili waweze kulipwa na mafao yao ya uzeeni? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kwanza, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Kamonga, kwamba kwa utaratibu wa ajira ulioanza mwaka wa fedha 2021/2022. Kwanza ajira zinaombwa kwa njia ya mtandao kwa maana kwa njia ya kielektroniki. Kuna mfumo mahususi wa ajira lakini wanaoomba ajira wanaomba kituo mahsusi kwa maana ya ndani ya halmashauri husika na kituo husika.

Mheshimiwa Spika, tumeshaweka utaratibu kwamba, lazima waripoti na hawawezi kuhamishwa ndani ya miaka mitatu ya kwanza katika maeneo yao. Naomba kuchukua suala hili la Ludewa, tulifanyie ufuatiliaji kama kuna madaktari walipangiwa na kabla hawajaripoti walihamishwa, tuone ni kwa sababu gani hatua hizo zilichukuliwa kinyume na taratibu za ajira ambazo zimewekwa kwenye mfumo wa ajira kukaa angalau miaka mitatu.

Mheshimiwa Spika, tutaendelea kuhakikisha kwamba halmashauri zote za pembezoni, zinapangiwa watumishi zaidi kuliko za mijini kwa sababu za pembezoni zina upungufu mkubwa. Tutahakikisha kwamba hatuhamishi bila sababu za msingi kwa watumishi kutoka halmashauri za pembezoni.

Mheshimiwa Spika, kuhusu wananchi kuajiri walinzi katika shule na maeneo mengine kama zahanati. Tulielekeza kwamba Serikali za Vijiji ziweke utaratibu rafiki kwa wananchi kuona uwezekano wa kulinda rasilimali za shule. Lakini zahanati na vituo vingine vya huduma bila kuwaumiza wale walinzi kwa maana kuwalipa posho zao na kuhakikisha kwamba wanawekewa fedha kwa ajili ya kiinua mgongo pale wanapostaafu kwa taratibu zile za ajira za mikataba, ahsante. (Makofi)

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha Wilayani Ludewa hususan eneo la elimu, afya na uvuvi?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia fursa hii. Jimbo la Newala Vijijini lina jumla ya walimu 475 kati ya walimu 787 wanaohitajika kuwepo.

Je, ni lini Serikali itapeleka walimu 312 ambao ni upungufu katika Jimbo la Newala Vijijini? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuajiri watumishi wa Kada ya Elimu na pia imeendelea kupeleka walimu katika Halmashairi ya Newala Vijijini lakini tunatambua kwamba bado kuna upungufu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba kadri Serikali itakavyokuwa inaajiri walimu, tutatoa kipaumbele katika Halmashauri ya Newala Vijijini. Ahsante.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha Wilayani Ludewa hususan eneo la elimu, afya na uvuvi?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ina upungufu wa watumishi wa Sekta ya Afya takribani asilimia 60 ya mahitaji yake.

Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka miwili ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kazi kubwa sana ya kuajiri wataalam wa afya imefanyika. Jumla ya watumishi wa kada mbalimbali za afya wapatao 17,000 wameajiriwa na kupelekwa katika halmashauri zote kote nchini ikiwepo Halmashauri ya Mji wa Nanyamba.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu bado kuna upungufu, namuhakikishia Mheshimiwa Mbunge, kwamba kadri tutakavyoendelea na ajira nyingine za wataalam wa afya, tutatoa kipaumbele kwa Halmashauri ya Mji wa Nanyamba. ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha Wilayani Ludewa hususan eneo la elimu, afya na uvuvi?

Supplementary Question 4

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi. Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika ina upungufu wa watumishi wa kada ya ualimu wapatao 1000 na kada ya afya wapatao zaidi ya 200.

Je, ni lini Serikali itaenda kutatua kero ya watumishi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, utatuzi wa changamoto ya upungufu wa wataalam wa sekta ya elimu na afya ni mchakato, safari ni hatua, tumeanza. Katika Halmashauri ya Tanganyika nafahamu ni moja ya halmashauri ambazo zilipata watumishi wengi sana katika ajira mbili zilizopita ukilinganisha na halmashauri nyingine kwa sababu ya vigezo vya kuwa ipo mbali zaidi lakini ilikuwa na upungufu mkubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba zoezi ambalo limeanza la kupeleka watumishi kwa wingi Tanganyika, litaendelea kadri tutakavyokuwa tunaendelea kuajiri watumishi wa sekta hizo. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha Wilayani Ludewa hususan eneo la elimu, afya na uvuvi?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuweza kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa walimu katika shule za msingi na sekondari Mkoa wa Simiyu hasa walimu wa sayansi; je, ni lini Serikali itapeleka walimu wa kutosha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa 11 ambayo Ofisi ya Rais - TAMISEMI iliiainisha ikiwa ni mikoa yenye upungufu mkubwa zaidi wa watumishi wa sekta ya elimu, lakini pia wa sekta ya afya. Kila ajira zinapotokea, mikoa hii inapewa kipaumbele cha hali ya juu zaidi kuliko mikoa mingine ambayo ina nafuu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo ajira mbili zilizopita walivyopata watumishi wengi Mkoa wa Simiyu, tutaendelea kupeleka watumishi wengi ili waweze kupunguza pengo la watumishi katika vituo lakini na shule zetu, ahsante.