Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 123 2023-09-08

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha Wilayani Ludewa hususan eneo la elimu, afya na uvuvi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Jimbo la Ludewa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa ikama ya mwaka 2022/2023 Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa inahitaji jumla ya watumishi 3,327. Watumishi waliopo ni 1,985 hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 1,342 sawa na asilimia 40.33.

Mheshimiwa Spika, mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali iliajiri jumla ya wataalam 149 wa kada za afya, elimu msingi, sekondari na uvuvi na kuwapangia Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa. Serikali inatambua upungufu huo wa watumishi na itaendelea kuajiri wataalam wa kada mbalimbali na kuwapanga kwenye maeneo yenye mahitaji kote nchini ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, ahsante.