Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa semina elekezi kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya mara kwa mara kuhusu utawala bora?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kutokana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, tunakubaliana kwamba semina elekezi ni muhimu mara baada tu ya kuteuliwa. Nina swali moja tu la nyongeza.

Kwa kuwa ripoti ya Tume ya Haki Jinai iliyotolewa hivi karibuni, imezungumzia matumizi mabaya ya waliopewa mamlaka, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa, namna wanavyotumia masaa 24 kuwaweka watu ndani bila kufuata taratibu.

Je, ni lini Serikali italeta Mswada hapa Bungeni ili tufanye marekebisho kuwaondolea hayo mamlaka wabaki kuwa wasimamizi wa shughuli za maendeleo na yabaki kwa Jeshi la Polisi pekeyake? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ni ukweli kuwa kwamba sasa Serikali imekwisha toa tayari taarifa ya kijinai, na kwamba taarifa hiyo imekwisha anza kufanyiwa kazi na wananchi wanashirikishwa katika maeneo mbalilmbali ili kuweza kutoa maoni yao na baada ya hapo taratibu nyingine za mabadiliko ya sheria ziweze kufuatwa.

Mheshimiwa Spika, namuomba mheshimiwa Mbunge na Bunge lako liwe na Subira wakati mchakato wa kuendelea kukusanya maoni ya watu yanaendelea kupatikana ili itakapokuwa tayari sasa tuweze kuleta; na kama kutakuwa na mapendekezo ya mabadiliko ya sheria na kama kutakuwa na miongozo yeyote ile sisi kama Serikali au nchi tuweze kuifanyia kazi, ahsante.

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa semina elekezi kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya mara kwa mara kuhusu utawala bora?

Supplementary Question 2

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itarejesha utaratibu wa mafunzo elekezi ya uongozi, utawala bora na uadilifu kwa watumishi ambao wamefikia ngazi ya Afisa Mkuu ili wanapopata nafasi za uteuzi waweze kutumika ipasavyo? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma na Sheria ya Utumishi wa Umma pia Ibara ya 4 hadi Ibara ya 8 inampa mamlaka Katibu Mkuu Kiongozi kuweza kuhakikisha kwamba utumishi wa umma unakuwa ulio bora na ambao unakwenda na weledi lakini pia ambao unaweza kuwahudumia wananchi.

Mheshimiwa Spika, nataka kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako, kwamba Serikali imeendelea kufanya utaratibu wa kutoa mafunzo kwa watendaji wote au watumishi wote ambao wanakuwa katika ngazi za uteuzi ili kuweza kuwa katika viwango bora vya kutoa huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, nataka kumhakikishia kwamba hilo jambo au maombi ya Mheshimiwa Mbunge tutaendelea kuyafanyia kazi na tutaendelea kuhakikisha kwamba tunakuwa na utumishi ulio bora kama ambavyo sheria inamtaka Katibu Mkuu Kiongozi.