Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 115 2023-09-07

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa semina elekezi kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya mara kwa mara kuhusu utawala bora?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa mafunzo elekezi kwa viongozi wa ngazi mbalimbali katika kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeendelea kutoa semina elekezi kwa viongozi wanaoteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo. Katika kipindi cha mwezi Februari hadi Agosti, 2023, Serikali ilitoa mafunzo elekezi kwa viongozi wa ngazi ya Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala wa Wilaya ambapo agenda moja wapo ilikuwa ni ya utawala bora.