Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Iwondo umefikia asilimia 80 lakini fedha za kumalizia asilimia 20 iliyobaki zimekwisha. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa kituo hicho ili wananchi wa kata hiyo waweze kupata huduma?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kituo cha Afya cha Kata ya Matomondo kimekamilika na sasa kinatoa huduma lakini kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi na hasa kada ya madaktari. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi katika kituo hicho cha afya ili wananchi wa Kata ya Matomondo waweze kufurahia huduma ya afya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa kwamba Serikali inajenga vituo hivi vya afya kwa awamu. Niwapongeza kwa kujenga kituo cha afya hiki cha Iwondo mpaka kufikia hatua ya asilimia 80 na bado asilimia 20 ya fedha kwa ajili ya ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, nitoe wito kwa Mkurugenzi wa Halmashauri kufanya mahesabu tufahamu hii asilimia 20 iliyobaki ni sawa na shilingi ngapi ili tuweze kuona namna ya kupata fedha Serikali Kuu pia na namna ya kupata fedha kutoka kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya kukamailisha ujenzi wa kituo hiki cha afya.

Mheshimiwa Spika, pili, kituo cha afya ambacho kinatoa huduma, Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt, Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha miaka miwili na nusu imeajiri jumla ya watumishi wa sekta ya afya wapatao 17,000 ambao wamepangwa katika vituo mbalimbali kikiwepo kituo hiki. Zoezi hili ni endelevu na tutatoa kipaumbele kwa ajili ya kituo hiki cha afya cha Mpwapwa, ahsante.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kata ya Igamba katika Wilaya ya Mbozi ni moja ya kata ambazo zimeahidiwa kupelekewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya. Je, ni lini sasa hizo fedha zitaenda ili ujenzi uanze?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kata hii ya Igamba itapelekewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kama ambavyo Serikali imeahidi, ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha afya katika Kata ya kimkakati ya Kandawale? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati katika Kata zetu zote nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali imefanya tathmini na kuainisha maeneo ambayo yana sifa ya kuwa na vituo vya afya vya kimkakati na tutakwenda kujenga vituo hivi vya afya kwa awamu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nakuhakikishia kwamba itakapofikika awamu hiyo tutawapatia fedha kwa ajili ya kujenga kituo hicho cha afya, ahsante sana. (Makofi)

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 4

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona. Katika Wilaya ya Chunya zipo Kata chache za kimkakati ambazo hazina vituo vya afya. Je, ni lini Serikali itatenga na kupeleka fedha kwa ajili ya kujenga vituo vya afya kwenye Kata za Luwalaje, Upendo na Kata ya Chokaa katika Kijiji cha Mapogoro? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nampongeza Mheshimiwa Mbunge wa Chunya kwa kuwa na taarifa ya vituo vyake vya kimkakati kama walivyo Waheshimiwa Wabunge wengine. Wameshazileta Ofisi ya Rais, TAMISEMI Serikali inaendelea kutafuta fedha ili ujenzi kwa awamu katika maeneo haya ufanyike. Tutatoa kipaumbele katika Kata ambazo umezitaja, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, Kata za Suji, Vudee na Mshewa ni Kata za kimkakati; je, ni lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata hizo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza kujenga vituo vya afya hivi vya kimkakati katika maeneo ambayo ameyataja. Nitoe wito na kusisitiza kwamba ni wajibu wa halmashauri kupitia Wakurugenzi na Mabaraza ya Madiwani kuanza kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kuanza ujenzi huu na Serikali Kuu itachangia kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana, ahsante. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 6

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mmepeleka fedha shilingi milioni 500 na mmechukua milioni 300. Je ni lini inapeleka fedha kwa ajili ya kumaliza kituo cha afya cha Maretadu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu DC, ambako fedha ya Serikali shilingi milioni 500 ilipelekwa kwa ajili ya kujenga kituo cha afya lakini kwa maamuzi ya Mkurugenzi na Baraza la Madiwani walikiuka utaratibu wakahamisha shilingi milioni 300 kutoka kituo cha afya wakapeleka kwenye mradi mwingine wa hospitali ya wilaya.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi wa Mbulu Vijijini kuhakikisha shilingi milioni 300 waliyoihamisha bila kufuata utaratibu inarejeshwa kwenye kituo cha afya na kukamilisha kituo cha afya kwa haraka iwezekanavyo na sisi ofisi ya Rais, TAMISEMI tutafuatilia, ahsante. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 7

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kubadilisha Zahanati ya Reguruki iiliyoko Jimbo la Arumeru Mashariki kuwa kituo cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Serikali imekuwa na utaratibu wa kupandisha hadhi zahanati ambazo zipo katika maeneo yanayokidhi vigezo vya kuwa vituo vya afya. Kwa hiyo, naomba nipokee hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwa zahanati hii ya Reguruki ili tuweze kufanya tathmini na kuona ni kwa kiasi gani anakidhi vigezo vya kuwa kituo cha afya na Serikali ichukue hatua kwa ajili ya kupandisha hadhi, ahsante.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 8

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya Kuuliza swali la nyongeza. Rais wa Awamu ya Tano wakati wa uhai wake alipokuwa katika ziara Wilaya ya Tunduru aliahidi ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Namihungo. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais ya ujenzi wa kituo cha afya katika kituo cha Namihungo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ahadi za Viongozi wetu wakuu wa kitaifa ni kipaumbele katika utekelezaji wa miradi hiyo kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Nachukua hoja hii, tayari najua tumeshaanza kuiratibu na tunatafuta fedha na mara fedha zikipatikana tutaleta shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga kituo hiki cha afya, ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 9

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa kuwa mimi bado natafuta vituo vitatu vya tarafa, lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya vituo vya tarafa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nakushukuru, naomba tu kumuhakikishia Mheshimiwa Mbunge wa Kiteto kwamba, pamoja na yeye, bado kuna baadhi ya majimbo pia na wilaya zetu ambazo tarafa nzima haina kituo cha afya. Tunafanya mpango wa kuhakikisha kwamba tarafa zote ambazo zina idadi kubwa ya wananchi na kuwa na umbali mrefu kutoka kituo kingine zinapewa kipaumbele kwenye vituo vya afya vya kimkakati. Kwa hiyo nikuhakikishie kwamba tarafa ulizozitaja zitapewa kipaumbele kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 10

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Serikali iliahidi kutuma wataalam kwenda kufanya tathmini na uchambuzi ili kijengwe kituo cha afya Kata ya Likawage Jimbo la Kilwa Kusini.

Je, ni lini wataalam hawa watakwenda kufanya tathmini hii ili kituo hicho kijengwe mara moja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Suala hili lipo ndani ya uwezo wa wataalam wa Mkoa wa Lindi. Tuna Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi na tuna Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilwa. Natoa maelekezo, ndani ya siku 14 wawe wamefanya tathmini ya vigezo kama tunahitaji kujenga kituo cha afya hapo lakini wawasilishe Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tufanye maamuzi kwa ajili ya kuanza kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi. Nashukuru.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 11

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwa kuwa kata ya Ikuna ni miongoni mwa kata za kimkakati na ni kata ambayo ina wakazi wengi, na wananchi wameshaanza kujenga kituo cha afya kwa nguvu zao zaidi ya miaka miwili.

Je, ni lini Serikali itatupatia kiwango cha fedha ili tumalizie kituo hicho cha afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, nawapongeza wananchi wa Kata hii ya Ikuna kwa kuanza kujenga kituo cha afya kwa nguvu zao. Tutakwenda kuchangia nguvu za wananchi kumalizia kituo hichi cha afya baada ya kufanya tathmini ya kuona hatua waliyofika na kiasi gani cha fedha kinahitajika. Lakini pia nimuombe Mkurugenzi wa Halmashauri atenge fedha pia za mapato ya ndani wakati tunatafuta fedha za Serikali Kuu. Ahsante.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Supplementary Question 12

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, je, ni lini Serikali itajenga upya ama kukarabati jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika Kituo cha Afya Likombe kilichopo Manispaa ya Mtwara Mikindani? Jengo hilo limechakaa, na la zamani, halikidhi mahitaji ya sasa.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kutumia fursa hii kumuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI tathmini ya gharama zinazohitajika kwenye kufanya ukarabati lakini pia kama ni kufanya ujenzi mpya, ili tuweze kuona kama gharama hiyo ipo ndani ya uwezo wa mapato ya ndani ya Halmashauri. Tutatoa maelekezo ili waanze kutenga fedha mwaka wa fedha 2024/2025. Kama ipo nje ya uwezo wao, Ofisi ya Rais TAMISEMI, kwa maana ya Serikali Kuu, itaangalia namna ya kuwaunga mkono kupitia fedha ya Serikali Kuu.