Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 113 2023-09-07

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga vituo vya afya katika Kata za Mlembule, Godegode, Chunyu na Berege – Mpwapwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Natany Malima, Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mahitaji ya vituo vya afya katika Kata za kimkakati kote nchini. Katika kipindi cha miaka mitano Serikali imetekeleza ujenzi wa vituo vipatavyo 2,406 vya kutolea huduma za afya ambavyo bado vina uhitaji wa baadhi ya miundombinu ikiwemo vifaa tiba na watumishi.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga kwa awamu fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kwenye maeneo ya kimkakati kote nchini ikiwemo Kata za Godegode, Chunyu na Berege katika Halmashauri ya Mpwapwa, ahsante.