Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza:- Je, lini Shirika la Ndege Tanzania litaanza safari za Pemba?

Supplementary Question 1

MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali yenye kutia matumaini, lakini nimuulize swali la nyongeza.

Je, haoni kama ipo sababu ya kuweza kuweka kipaumbele au Wizara yake iko tayari kutoa kipaumbele kwa hili jambo ili kuweza kutatuliwa kwa haraka sana, kwa sababu Wapemba wanalaghaiwa na issue hii imekuwa kubwa sana. Sasa hivi ili Wapemba waweze kukupa dua ili uweze kutoboa katika mikeka ijayo?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Salim Mussa Omar kwamba Serikali inafahamu na inatambua uzito mkubwa na umuhimu wa kupeleka ndege hiyo Pemba na ndiyo maana imeshaanza mchakato. Alichokifanya ni kutukumbusha, nasi tutajitahidi kuongeza kasi zaidi ili angalau ndugu zetu Wapemba waweze kusafiri kama inavyotakiwa. (Makofi)

Name

Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza:- Je, lini Shirika la Ndege Tanzania litaanza safari za Pemba?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Singida ni jirani kabisa na Mkoa wa Dodoma ambao ndiyo Makao Makuu ya nchi: Je, ni lini Kiwanja cha Ndege Singida kitakamilika ili wananchi wa Singida wapate huduma; lakini pia uwanja huo wa Singida utumike kama uwanja wa dharura kama Dodoma kuna changamoto? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Singida ni mkoa ambao uko karibu na Dodoma na Serikali tayari imeshafanya usanifu wa Uwanja wa Singida ili uweze kujengwa, kwani unaweza ukatumika sana pale ambapo kunatokea changamoto katika viwanja vya Mkoa wa Dodoma, ahsante. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi kwa kunisaidia. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya usanifu kukamilika, hatua inayofuata sasa ni kujua mahitaji halisi kwa ajili ya fidia ili hatimaye tuweze kuanza kufanyia kazi huo uwanja. (Makofi)