Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 73 2023-09-04

Name

Salim Mussa Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Gando

Primary Question

MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza:-

Je, lini Shirika la Ndege Tanzania litaanza safari za Pemba?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kutujalia afya njema. Pili, kwa sababu ninasimama kwa mara ya kwanza hapa, nitumie nafasi hii kwa unyenyekevu mkubwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuniamini na kuniteua kuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi. Kwa unyenyekevu mkubwa nimepokea uteuzi huu na ninaahidi kufanyakazi kwa juhudi, maarifa kwa ajili ya maslahi makubwa ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kipekee ninakushukuru wewe kama mlezi na Kiongozi wangu kwa ushirikiano mkubwa ulionipatia nikiwa Msaidizi wako kwa nafasi ya Mwenyeketi wa Bunge na Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda, Kilimo na Mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, ninaomba sasa kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi kujibu swali la Mheshimiwa Salimu Mussa Omar, Mbunge wa Gando, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ATCL itaanza safari za Pemba baada ya kupata ndege za kutosha kuweza kutoa huduma bila kuharibu ratiba za safari za sasa na urukaji kwa wakati. Kwa kuwa mwisho wa Septemba, 2023 ATCL inatarajia kupata ndege mpya moja aina ya Boeing B737-9MAX na ndege ndogo aina ya Dash 8 Q300 matengenezo yake yanatarajiwa kuwa yamekamilika na kurejea katika ratiba zake za utoaji wa huduma. Uwepo wa ndege hizo kutaiwezesha ATCL kuanzisha safari zake katika kituo cha Pemba kwa tija na ufanisi mkubwa.