Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, lini Serikali itaanzisha Mfuko wa Fidia kwa wahanga wanaoathirika na wanyamapori wakali na waharibifu?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikitoa kifuta jasho kwa wahanga walioathirika na wanyamapori ikiwepo laki moja tu kwa heka nzima ya mazao yaliyoharibiwa au shilingi laki mbili kwa mtu aliyejeruhiwa, laki tano kwa aliyepata jeraha la kudumu na labda milioni moja kwa familia ya aliyeuawa na wanyama pori na pengine kuchelewesha kutoa malipo hayo kwa wahanga.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu matukio hayo yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku pengine kuwa mzigo mkubwa kwa Serikali na kushindwa kuwalipa kama ilivyo nchi ya jirani ni kwa nini sasa Serikali isione umuhimu wa kuanzisha huu mfuko wa fidia kwa wahanga?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Serikali yetu ya Tanzania bado inatoa kifuta jasho kwa wahanga, haioni sasa ni muda mwafaka kurejea na kubadilisha baadhi ya mafungu katika Sheria hiyo ya Wanyamapori ya mwaka 2011 hasa kuongeza nyongeza hii ya fidia angalau iendane na hali ya maisha ya sasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli imekuwepo changamoto ya viwango vya fidia au kifuta jasho kuwa vidogo. Vilevile ni kweli kwamba wakati mwingine imechukua muda mrefu kwa wananchi hao kufidiwa. Serikali imeliona hili na imelifanyia kazi na tuko kwenye hatua za mwisho za kuona kwamba kanuni zinafanyiwa marekebisho ili wananchi waweze kulipwa stahiki zao kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na hili la kusema tuanzishe mfuko maalum. Serikali imefanyia kazi jambo hili na imefanya utafiti kwa nchi jirani ambazo zimekuwa na mfumo huu na imejiridhisha kwamba wenzetu wamepata matatizo kuendana na mfumo huu unaopendekezwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali inajielekeza kuweka mikakati ya dharula ambayo itatuhakikishia kwamba tunaondokana na tatizo hili, nakushukuru.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, lini Serikali itaanzisha Mfuko wa Fidia kwa wahanga wanaoathirika na wanyamapori wakali na waharibifu?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi. Wako wananchi wangu wa Kata ya Maore, Karemawe, Bendera nakadhalika ambao wameuawa na Tembo takribani miaka miwili sasa lakini Serikali haijatoa kifutajasho wala chochote.

Je, hauoni kwamba Serikali inaonekana kama inawathamini Tembo zaidi kuliko ambavyo inawaona wananchi?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imechukulia kwa umuhimu na uzito mkubwa maisha ya Watanzania. Kutokana na changamoto hizi ambazo zimekuwa zikijitokeza kwa tembo kuvamia na kupoteza maisha ya wananchi wetu, Serikali imeandaa mkakati wa dharura ambao utatuondoa kwenye changamoto hii. Naomba tuipe Serikali muda, ndani ya kipindi mfupi tutaona matokeo ya utekelezaji wa jambo hili.