Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 65 2023-09-04

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanzisha Mfuko wa Fidia kwa wahanga wanaoathirika na wanyamapori wakali na waharibifu?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la kama ulivyonielekeza.

Mheshimiwa Spika, kwa hii ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako tukufu baada ya Mheshimiwa Rais kunipa heshima hii ya kuniteua kuwa Naibu Waziri, naomba nitumie fursa hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema ambaye imempendeza niweze kutumika kwenye nafasi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pili nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kunipa heshima hii ya kuitumikia nchi yetu. Naahidi kutekeleza majukumu yangu kwa uwezo wangu wote na kwa vipawa vyote alivyonipa Mwenyezi Mungu, naahidi sitamwangusha.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba ushirikiano wako na Wabunge wenzangu nawaahidi ushirikiano naomba tushirikiane. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikilipa kifuta jasho na kifuta machozi kama mkono wa pole au faraja kwa wananchi wanaopata madhara kutokana na wanyamapori wakali na waharibifu. Malipo hayo yamekuwa yakifanyika kwa mujibu wa Kanuni za Kifuta Jasho na Machozi za mwaka 2011 na kwa kadri ya upatikanaji wa fedha hizo.

Mheshimiwa Spika, kanuni hizo zilianza kutekelezwa mwaka 2012 ambapo katika kipindi cha kuanzia 2012/2013 hadi 2022/2023 jumla ya shilingi bilioni 11.3 zimelipwa kwa wananchi walioathiriwa na wanyamapori wakali na waharibifu. Hata hivyo, suala hili limekuwa ni changamoto kubwa kwa nchi nyingi za Afrika ambapo limesababisha baadhi ya nchi kuondokana na utaratibu wa kulipa kifuta jasho na machozi. Lakini Tanzania imeendelea kuona umuhimu wa kuwafuta jasho na machozi wananchi kwa madhara wanayoyapata kutokana na wanyamapori hao. (Makofi)