Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Napenda kujua kama ratiba ya kukamilisha mradi mkubwa wa maji kutoka Mwanga kwenda Same mpaka Korogwe imebaki pale pale mpaka mwaka kesho mwezi wa Nne wananchi wa Same wanapata maji kutoka Mwanga?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa sasa hivi wananchi wangu wa Same hawana maji: Serikali ina mpango gani wa dharura kuchimba visima virefu katika Kijiji cha Ishire, Kitongoji cha Kavambuhu, Majevu, Kirinjiko, Makanya pamoja na Mabilioni?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza. Wizara tutafanya kila jitihada kuhakikisha mradi huu unakamilika ndani ya wakati kadiri tulivyosaini mkataba na mkandarasi.

Mheshimiwa Spika, kwa suala la dharura, maeneo yote yenye dharura kama Same Mjini na hasa maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Mathayo, tutafanya kila jitihada kuona mashine ambazo Mheshimiwa Rais ametununulia tuweze kuondoa changamoto hii, basi tutakwenda kuchimba hivi visima. Lengo ni wananchi kupata huduma kwa wakati.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wananchi wa Kiegea, Mkundi pamoja na Kilimanjaro bado hawapati maji ya kutosha; je, ni lini watapata maji ya kutosha kutoka kwenye mradi wa Mguu wa Ndege? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Christine. Huu mradi mimi na yeye akiwa Mwenyekiti wa Kamati tulifika na kuufuatilia kwa karibu sana na anaendelea kuufuatilia. Mpaka sasa tumeshaweza kutekeleza mradi kwa asilimia 86. Maeneo ya Kihonda Kaskazini na Kilimanjaro, hivi navyoongea tayari wameshaanza kupata huduma.

Mheshimiwa Spika, maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Dkt. Christine na yenyewe pia tunaendelea kufanya jitihada kuona kwamba kufikia Desemba, mwaka huu 2023 na yenyewe pia yaweze kupata huduma ya uhakika.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 3

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mji wa Nyeunge una idadi kubwa sana ya watu na unahudumiwa na mradi wa maji wa Rumea, Karebezo hadi Nyeunge ambao ulijengwa chini ya kiwango; je, Serikali iko tayari kuufanyia kazi mradi huu ili uweze kutoa huduma ya uhakika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Eric Shigongo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala hili la ukarabati wa mradi, Mheshimiwa Mbunge ameshafika ofisini na tumeweza kuongea pamoja na wataalam. Naomba nimhakikishie, tulivyomuahidi mradi huu ni lazima tunakwenda kuutekeleza na tutahakikisha ukarabati uwe na tija na huduma inayotarajiwa ya maji safi na salama bombani iweze kupatikana kwa wakati.

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 4

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Ni lini Serikali itapeleka fedha kwenye miradi ya Itununu, Tabweta ili iweze kukamilika na wananchi wa Tarime wapate maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi hii aliyoitaja ipo katika mpango wa kulipa fedha katika miezi hii ya Julai na Agosti. Fedha zimechelewa kufika, lakini kuanzia wiki hii wakandarasi wapo kwenye utaratibu wa kuweza kulipwa kwa lengo la kuendelea na utekelezaji wa miradi hii.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 5

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Jiji la Dodoma limeendelea kukumbwa na kadhia kubwa ya uhaba wa maji: Je, Serikali ni lini mtakamilisha mradi wa visima vya Nzuguni ili kuondoa kadhia hii inayowakumba wananchi na wakazi wa Jiji la Dodoma? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti Majala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ukamilishaji wa visima vya Nzuguni, kadiri tunavyopata fedha tutaendelea kumwezesha mkandarasi ili viweze kukamilika ndani ya miezi ya mkataba tuliyokubaliana naye. Tunafahamu changamoto kubwa inayokumba Jiji la Dodoma na tunaendelea na jitihada nyingi sana kuona kwamba pamoja na visima hivi na vyanzo vingine, tuweze kuondoa adha ambayo ipo kwenye Jiji la Dodoma.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, kwanza niruhusu nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa fursa ambayo nimeipata kuja kuuliza swali hapa. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa imani yake kubwa kwa kuniamini, nimefanya kazi na nimetua kijiti kwa Mheshimiwa Silaa na niko tayari kutoa ushirikiano wakati wowote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina swali la nyongeza. Kwanza natambua kwamba Serikali imeweka katika bejeti yake kuongeza chanzo kingine cha maji katika Jiji la Mwanza, hususan Manispaa ya Ilemela kutokana na changamoto kubwa ya maji katika mji ule: Je, ni lini utekelezaji wa mradi huo wa chanzo kipya cha maji utaanza kutekelezwa? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Angeline Mabula Mbunge wa Ilemela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nipende kumpongeza kwa sababu suala hili amesha lileta mara kadhaa katika ofisi zetu na niseme tu jitihada zako zimesababisha Mheshimiwa Waziri Jumaa Hamidu Aweso kukuletea Mkurugenzi wa mamlaka mpya mwanamama, mchapakazi. Jitihada zako zimesababisha kuileta task force ya wataalam kuona kwamba Mwanza sasa inaenda kupata suluhu.

Mheshimiwa Spika, chanzo hiki kipya Mheshimiwa Dkt. Angeline Mabula naomba nikupe amani kwamba kadri wataalam wetu watakapo kamilisha kazi waliyopewa na Mheshimiwa Waziri Jumaa Hamidu Aweso, chanzo hiki mara moja kinakwenda kufanyiwa kazi ndani ya mwaka huu wa fedha.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Supplementary Question 7

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi hii. Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu imechimbiwa visima zaidi ya kumi na tano lakini hadi sasa havijapata pump ya kuendesha visima hivyo. Je, ni lini Serikali itatoa fedha ili visima vyote ambavyo vimechimbwa ndani ya jimbo langu viweze kufanya kazi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, visima vilivyoko Nanyumbu tunavishughulikia na manunuzi ya pump yako kwenye hatua za mwisho.