Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 63 2023-09-04

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa maji tambarare ya Same wakati ukisubiriwa Mradi wa Maji wa Mwanga – Same hadi Korogwe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wakati utekelezaji wa mradi mkubwa wa Same – Mwanga – Korogwe unaendelea na unaotarajia kukamilika mwezi Juni, 2024 na kunufaisha baadhi ya maeneo ya Wilaya za Same, Mwanga na Korogwe, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kutatua changamoto ya maji kwa wananchi wa Wilaya ya Same. Mathalani katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imekamilisha miradi ya maji katika Vijiji vya Kirinjiko, Mabilioni Kijomo na Gunge na tayari inatoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi. Aidha, visima vitatu vimechimbwa katika eneo la Mahuu kwa ajili ya kuhudumia eneo la Same Mjini ambapo kwa jumla vina uwezo wa kuzalisha jumla ya lita 720,000 kwa siku.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka huu wa fedha 2023/2024, Serikali itafanya utafiti wa maji chini ya ardhi pamoja na kuchimba visima virefu viwili katika maeneo ya Same Mjini na Kijiji cha Marondwe, Njoro ili kuongeza vyanzo zaidi vya maji. Utekelezaji wa visima hivyo unatarajiwa kuanza mwezi Januari, 2024 mara baada ya uchimbaji kukamilika na maji kupatikana.