Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko kubwa la Samaki Lindi Manispaa?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu hayo ya Serikali yenye kuleta matumaini kwa wananchi wa Lindi Manispaa. Hata hivyo, naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Lindi Manispaa tumeshatenga ekari moja na nusu kwa ajili ya ujenzi wa soko hili la samaki, vilevile tuna wavuvi 2,193 ambao wamesajiliwa na wachuuzi wadogo wadogo 470 ambao wanakosa mahali pa kufanyia shughuli zao za biashara. Naomba Serikali itupe majibu ya uhakika na ya kueleweka ya kuwapa wananchi wa Lindi Manispaa matumaini; ni lini sasa mtaanza kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa soko la Samaki?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake kwa wavuvi kwa kuwakopesha maboti, pamoja na nyavu na injini ili wavuvi hawa sasa waendeleze uvuvi wao kwa vifaa hivi vyenye uhakika na usalama wa kutosha? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa Mbunge alivyouliza swali lake la nyongeza kuwa tayari Halmashauri ya Manispaa ya Lindi tayari wameshakupata eneo, namwomba baada ya Bunge hili twende na wataalamu pale Lindi tukahakiki hilo eneo na wataalamu na tukishajua eneo hilo lililopatikana lina ukubwa gani na linafaa kwa matumizi hayo, Wizara iko tayari kuanza ujenzi wa soko hilo mara moja.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameuliza kuhusu zana. Tathmini tayari imeshafanyika, wataalamu wameshafanya tathmini ya zana gani zinafaa kwa maeneo hayo ya wavuvi, namwomba baada ya hili, kwa sababu tayari kila kitu kimeshafanyika, basi baada ya Bunge hili tuambatane naye kama nilivyosema hapo awali, twende kwa wavuvi hao kuhakiki ni aina gani ya zana zinazohitajika ili Serikakli ione namna ya kuanza kuwakopesha wavuvi hao hizo zana, ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko kubwa la Samaki Lindi Manispaa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Ni lini Serikali itaanza mpango wa kujenga soko jipya la kisasa la samaki katika Wilaya ya Kigamboni?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, swali la nyongeza Mheshimiwa Ndugulile, anataka kujua ni lini Serikali itaanza ujenzi wa soko jipya Kigamboni. Ujenzi wa soko jipya Kigamboni utategemea uwezekano wa kibajeti. Kama Serikali itapata bajeti, basi iko tayati kuanza ujenzi wa soko hilo jipya pale Kigamboni, ahsante sana. (Makofi)

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko kubwa la Samaki Lindi Manispaa?

Supplementary Question 3

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, swali dogo la nyongeza. Hali ya soko la samaki Tanga ni sawa sawa kabisa na hali ya soko la samaki Lindi; je, ni upi mkakati wa Serikali katika kuhakikisha linapatikana soko la samaki la kisasa kwenye Jiji la Tanga?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge katika swali lake, wako wataalam wanafanya tathmini ya kuyatambua hayo masoko yote nchi nzima. Tunaomba nafasi ili wataalam hao waendelee na tathmini hiyo, na wakishamaliza, Serikali itatoa utaratibu wa namna gani masoko hayo yanakwenda kujengwa katika nchi yetu. (Makofi)

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga soko kubwa la Samaki Lindi Manispaa?

Supplementary Question 4

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Miundombinu ya soko la samaki katika Manispaa ya Mtwara Mikindani ni mibovu na mibaya hasa sehemu ya jiko pamoja na ofisi. Nini mkakati wa Serikali kuboresha miuondombinu hiyo? (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, soko la Mikindani ni kama masoko mengine ambayo nimeshatoa maelekezo, kwamba tutatuma wataalam kuja kuangalia upungufu uko wapi, halafu baada ya kuyajua huo upungufu, Serikali iko tayari kuanza kufanya marekebisho ya maeneo hayo. (Makofi)