Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 60 2023-09-04

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga soko kubwa la Samaki Lindi Manispaa?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama hapa naomba nitumie nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kila kitu, pia ninaamshukuru sana Mheshimiwa Rais Mama yetu Samia Hassan Suluhu kwa imani yake kubwa kwa kunipa nafasi hii nimsaidie kumuwakilisha katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya uvuvi nchini, ikiwemo masoko ya samaki katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi, kwa kuzingatia upatikanaji wa maeneo na rasilimali fedha. Changamoto iliyopo ni upatikanaji wa maeneo katika Halmashauri zetu kwa ajili ya ujenzi wa masoko. Kwa sababu hii, nimuombe Mheshimiwa Mbunge kwa nafasi yake, asaidie kupatikana kwa eneo la ujenzi wa soko hilo katika Manispaa ya Lindi na mara likipatikana, Wizara yangu itafanya tathmini za awali ikiwa ni pamoja na kuandaa michoro na gharama za ujenzi. Aidha, baada ya kukamilika kwa hatua hizo, Wizara itatafuta fedha za ujenzi wa soko hilo katika vyanzo vya ndani, yaani bajeti ya Wizara au miradi kwa ajili ya kuanza ujenzi.