Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 1

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri ametuambia kwamba wanatarajia kukamilisha mchakato wa zabuni mwezi Disemba, 2023.

Je, anaweza akatueleza leo kwamba ni lini wana mpango wa kutangaza tenda hii? Maana ili mchakato ukamilike lazima tenda iwe imetangazwa.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la nyongeza; Mradi huu wa TACTIC mpaka sasa ulishatangaza tender kwa ajili ya kujenga barabara za lami za Engo Sheraton, Olasiti pamoja na Oljoro ambapo tunakwenda kujenga stendi. Tender ilitangazwa tarehe 27 mwezi Februari, na deadline ilikuwa ni tarehe 14 mwezi wa Nne. Leo miezi mitano imeshapita lakini mkandarasi bado hajakwenda site.

Je, ni lini watampeleka mkandarasi site ili barabara hizi za lami za Engo Sheraton, Olasiti na Oljoro zianze kujengwa mara moja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza lini tunatangaza tenda hiyo; kama nilivyosema tupo kwenye hatua za utaratibu wa manunuzi na siwezi kuwa certain sana kusema lini exactily lakini nakuhakikishia tu kwamba by Disemba mwaka huu tutakuwa tumekamilisha taratibu zote za manunuzi, na mkandarasi kwenda site kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Spika, pili kuhusiana na hii tenda ya ujenzi wa barabara hizi ambazo mpaka sasa zaidi ya miezi minne, mitano mkandarasi hajaenda site. Naomba nitumie fursa hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, TAMISEMI, kutoa maelekezo kwa Meneja wa TARURA Mkoa wa Arusha, lakini pia Halmashauri ya Wilaya ya Arusha, kwa maana ya Jiji la Arusha, kuhakikisha wanamfuatilia mzabuni huyo kwa maana ya mkandarasi huyo aanze kazi mara moja kwa kufuata taratibu. Kama kuna mkwamo wowote Ofisi ya Rais- TAMISEMI tutaingilia kati kuhakikisha tunakwamua na kazi inaendelea, ahsante.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri unaonaje hilo agizo lako lingeenda kwa mameneja wote ambao mradi huo wa TACTIC unaenda?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, napokea na naomba niseme kuwa kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri naelekeza kwa Mameneja wote wa TARURA katika mikoa na wilaya ambazo zinatekeleza Mradi wa TACTIC kuhakikisha kuwa wanasimamia kwa karibu hatua zote za manunuzi, lakini pia kuhakikisha kuwa wakandarasi wanafika site kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi hiyo mara moja. Ahsante.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi nulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Soko na Stendi ya Kisongo Mateves ambayo ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Saputu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali imeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba, kwanza Halmashauri zenye miradi hiyo zinaainisha gharama zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi wa stendi na masoko hayo. Pia, kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya kuanza utekelezaji. Lakini kama gharama ni kubwa kuliko uwezo wa halmashauri, kuwasilisha Ofisi ya Rais-TAMISEMI kwa ajili ya utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, tutaenda kulitekeleza hilo, na hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais lazima tutaitekeleza na tutaipa kipaumbele katika miradi yetu ya ujenzi wa masoko na stendi.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi; ujenzi wa stendi Mji Mdogo wa Katesh unasuasua; je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kuwa stendi hiyo inakamilika haraka ili ianze kutumika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natoa maelekezo na nasisitiza kwa Mkurugenzi wa Halmashauri hii ya Hanang. Tulishafanya ziara pale, mimi na Mheshimiwa Mbunge lakini pia tuliona kweli stendi ile inasuasua. Tulitoa maelekezo na Halmashauri ilitoa commitment ya kuongeza fedha kwa ajili ya kukamilisha. Kwa hiyo, tunatoa maelekezo kwamba wahakikishe wanakamilisha stendi ile haraka iwezekanavyo na sisi Ofisi ya Rais-TAMISEMI tutafika kukagua na kuona kazi imetekelezwa kwa wakati, ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza upya mchakato wa ujenzi wa stendi ya kisasa eneo la Madira, mchakato huo ambao ulisitishwa mwaka 2019 ghafla wakati umefikia hatua ya utekelezaji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. John Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nilichukue hili suala la stendi hii ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja kule Arumeru tuone kwa nini ilisitishwa ghafla mwaka 2019, na hatua zipi zimechukuliwa kuondoa changamoto hiyo ili lengo la Serikali kuwahudumia wananchi kwa kujenga stendi hiyo liweze kukamilika kwa wakati.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 5

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Swali langu ni katika miji ile 45 na Makambako ipo; je, ni lini Serikali itaanza kujenga stendi na soko kwa Mji wa Makambako?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Mradi wa TACTIC katika Halmashauri ya Mji wa Makambako. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, nafahamu Makambako ipo awamu ya pili au ya tatu. Tunakwenda kusukuma kuhakikisha ujenzi wa stendi na soko katika Mji wa Makambako unaanza mapema iwezekanavyo. Najua taratibu za usanifu zimeshafanyika na zinaendelea kukamilishwa.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 6

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya mabasi katika Mji wa Babati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, stendi ya mabasi katika Mji wa Babati ni kipaumbele cha Serikali na tulielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Babati na Halmashauri ya Mji wa Babati zianze kuandaa na anafahamu, Halmashauri ya Mji wa Babati iko kwenye mpango wa TACTIC, na mpango huo wa TACTIC unaendelea kutekelezwa kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba tunakwenda kwa awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu na sasa zinakwenda sambamba kwa kufuatana. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Halmashauri ya Mji wa Babati ipo kwenye TACTIC, lakini kuhusu Halmashauri ya Wilaya ya Babati tutaendelea kuhakikisha kwamba Halmashauri inatenga lakini pia na sisi Serikali Kuu tunaona uwezekano wa ku-support.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 7

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Mbeya ni Jiji, lakini hauna stendi yenye hadhi ya jiji. Sasa je, ni lini Serikali itajenga stendi Mkoa wa Mbeya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mkoa wa Mbeya ni Jiji na jiji lile kwa bahati nzuri Mbunge wake ni Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson ambaye ni Spika wa Mbunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Serikali inatambua na imeweka kipaumbele kuhakikisha kwamba tunajenga stendi ya kisasa inayoendana na Jiji la Mbeya, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 8

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru, Halmashauri ya Wilaya wa Kilwa inaendelea na ujenzi wa Stendi ya Mabasi pale Nangurukuru, lakini uwezeshaji wake wa kimapato ni mdogo. Je, Serikali kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI, iko tayari sasa kuipa fedha Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ili ikamilishe ujenzi wa stendi pale Nangurukuru? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi ya mabasi Nangurukuru, ni kweli umeanza kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa. Naomba nitumie fursa hii kusisitiza kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilwa, kuhakikisha kwamba anaweka kipaumbele kwenye bajeti ya mapato ya ndani kuongeza kasi ya ujenzi wa stendi ile, lakini na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutafanya tathmini kuona kama wanashindwa, kwa maana ya uwezo wa mapato kukamilisha kwa wakati ili tuone uwezekano wa kupata fedha kwa ajili ya kuwa-support ili kuikamilisha kwa wakati, ahsante. (Makofi)

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya kisasa kwenye eneo la Bondeni City Jijini Arusha kupitia Mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 9

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii; je, ni lini sasa Serikali itajenga Stendi na Soko katika Halmashauri yangu ya Wilaya ya Mtwara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ujenzi wa stendi na soko katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara ni moja ya mahitaji ya wananchi na Serikali yetu ya Awamu ya Sita imeweka kipaumbele kusogeza huduma za kijamii kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, sasa nitumie fursa hii pia kuendelea kusisitiza kwamba ni wajibu wa Wakurugenzi wa Halmashauri husika kuweka vipaumbele kupitia mapato ya ndani, kuanza ujenzi wa stendi na soko. Halmashauri zetu nyingi zina uwezo wa kufanya hivyo zikiweka kipaumbele, lakini na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa maana ya Serikali Kuu tutaendelea kufanya tathmini na kuona maeneo ambayo yanahitaji kuongezewa nguvu, tutafanya hivyo ili stendi hizo na masoko yaweze kukamilika kwa wakati, ahsante. (Makofi)